Tuesday, May 21, 2013
KALI YA LEO: REAL MADRID WATELEKEZA BASI LAO LA KUSHEREHEKEA UBINGWA WA MFALME BAADA YA KUNYUKWA NA ATLETICO
Real Madrid walikuwa wakijiamini sana kuelekea fainali ya Ijumaa iliyopita ya Copa del Rey dhidi ya Atletico Madrid, lakini wapizani wao hao wakavunja uteja wa miaka 10 kwa kuwafunga Madrid na kubeba taji la kombe la mfalme.
Kutokana na kujiamini sana Madrid walikuwa wameshaandaa bus maalum kwa ajili ya kusherehekea ubingwa wao katika jiji la Madrid, lakini mambo yakawa tofauti wakafungwa na Atletico na matokeo yake wakaliacha bus lao la kusherehekea ubingwa likiwa tupu kwenye moja ya gareji moja iliyopo jijini humo.
Kwa upande wa Atletico wao wakalitumia bus lao kwa kutembeza kombe lao mbele ya maelfu ya washabiki ndani ya jiji la Madrid.
Kutokana na kujiamini sana Madrid walikuwa wameshaandaa bus maalum kwa ajili ya kusherehekea ubingwa wao katika jiji la Madrid, lakini mambo yakawa tofauti wakafungwa na Atletico na matokeo yake wakaliacha bus lao la kusherehekea ubingwa likiwa tupu kwenye moja ya gareji moja iliyopo jijini humo.
Kwa upande wa Atletico wao wakalitumia bus lao kwa kutembeza kombe lao mbele ya maelfu ya washabiki ndani ya jiji la Madrid.
HUU NDIO MCHANGANUO WA MAPATO YA VILABU VYA ENGLAND KUTOKA KWENYE MAUZO YA HAKI ZA TV - MAN UNITED WANAONGOZA
Manchester United kwa mara nyingine imeendelea kuwa kinara kwenye listi ya timu zinazoongoza kwa mapato makubwa kupitia haki za matangazo ya Television.
Mapato ya Premier League yanagawanywa kwa asilimia 50 za fedha zote kugawanywa sawa sawa kwa vilabu vyote, na pia mapato ya fedha kutoka nje ya nchi yanagawanywa kwa usawa.
Asilimia 25% ya mapato ya ndani yanagawanywa kutokana na ambapo timu imemaliza kwenye msimamo wa ligi, huku 25% zilizobakia zikitumika katika ya kiufundi katika kila mechi inayoonyeshwa kwenye TV ndani ya UK.
TIMU ZILIZOPATA MAPATO MENGI KWENYE EPL:
Man Utd £60.8m, Man City £58.1m, Arsenal £57.1m, Tottenham £55.8m, Chelsea £55m, Liverpool £54.8m, Everton £51.7m, West Ham £48.7m, West Brom £48.3m, Swansea £47.6m, Norwich £46.1m, Fulham £45.3m, Newcastle £45.1m, Aston Villa £44.9m, Stoke £44.5m, Southampton £43.8m, Sunderland £43.4m, Wigan £40.8m, Reading £40m, QPR £39.8m.
Mapato ya Premier League yanagawanywa kwa asilimia 50 za fedha zote kugawanywa sawa sawa kwa vilabu vyote, na pia mapato ya fedha kutoka nje ya nchi yanagawanywa kwa usawa.
Asilimia 25% ya mapato ya ndani yanagawanywa kutokana na ambapo timu imemaliza kwenye msimamo wa ligi, huku 25% zilizobakia zikitumika katika ya kiufundi katika kila mechi inayoonyeshwa kwenye TV ndani ya UK.
TIMU ZILIZOPATA MAPATO MENGI KWENYE EPL:
Man Utd £60.8m, Man City £58.1m, Arsenal £57.1m, Tottenham £55.8m, Chelsea £55m, Liverpool £54.8m, Everton £51.7m, West Ham £48.7m, West Brom £48.3m, Swansea £47.6m, Norwich £46.1m, Fulham £45.3m, Newcastle £45.1m, Aston Villa £44.9m, Stoke £44.5m, Southampton £43.8m, Sunderland £43.4m, Wigan £40.8m, Reading £40m, QPR £39.8m.
KOCHA SIMBA ATAJA SABABU ZA KUFUNGWA NA YANGA, ASEMA KIBARUA CHAKE SIMBA KIPO HATARINI
MUDA mfupi baada ya mechi ya watani wa jadi, Simba na Yanga wikiendi iliyopita, Kocha wa Simba, Patrick Liewig amesema hana uhakika na majaliwa yake lakini ametaja mambo manne yaliyoifanya timu yake ifungwe mabao 2-0 na Yanga.
Akizungumza katika mahojiano maalum, Liewig raia wa Ufaransa aliuambia mtandao huu kwamba, kikosi chake kilicheza vizuri lakini Yanga walitumia vizuri nafasi walizopata.
“Tulicheza vizuri kuanzia mwanzo hadi mwisho wa mchezo tatizo nafasi tulizopata hatukuzitumia vizuri na badala yake wenzetu Yanga walicheza vizuri na kutumia nafasi walizopata,” anasema Liewig.
Kocha huyo hata hivyo alisema anaamini kikosi chake kinachoundwa na wachezaji wengi vijana na wale waliokuwa hawapati nafasi kikosi cha kwanza, bado kina nguvu ya kufanya vizuri msimu ujao wa ligi na hata katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati ‘Kombe la Kagame’.
Liewig alitaja mambo makubwa manne yaliyoikwaza timu yake na kuruhusu kufungwa mabao 2-0 na Yanga;
SAIKOLOJIA;
“Kabla ya kuingia uwanjani si wachezaji tu hata mashabiki wetu wengi walijua timu yetu itafungwa, sasa kazi kubwa ilikuwa kuwaweka sawa wachezaji wetu hasa vijana katika hali ya kuhakikisha tunashinda mechi hii.
“Wakati sisi tukiwaza hivyo, wenzetu Yanga walikuwa wana uhakika wa ushindi na mbaya zaidi walikuwa wanawaza kuibuka na ushindi wa mabao mengi zaidi wakidhani kikosi chetu ni dhaifu,” anasema Liewig.
Liewig anakiri kwamba, pamoja na yote hayo lakini benchi la ufundi la Simba lilijitahidi kuwaweka sawa kisaikolojia lakini timu zilipoingia uwanjani ni wazi Yanga ilikuwa vizuri kisaikolojia katika ushindi kuliko wao.
PENALTI YA MUDDE;
Simba ilipata penalti dakika ya 28 baada ya beki wa Yanga, Nadir
Haroub ‘Cannavaro’ kumuangusha ndani ya eneo la hatari aliyekuwa mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa. Penalti hiyo ilipigwa na Mussa Mudde raia wa Uganda, lakini alikosa.
“Hadi tunapata penalti, Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0, hivyo kama tungepata penalti ile matokeo yangekuwa sawa na kuhamsha morali yetu ya kuhakikisha tunapata matokeo mazuri.
“Siku zote anayepiga penalti huwapa mashabiki uhakika wa kupata kwa asilimia kubwa, lakini Mudde amekosa na lile halikuwa lengo lake japokuwa umakini wa hali ya juu ulitakiwa kuwepo,” anasema Liewig.
KULINDA LANGO;
Liewig anasema kwa muda mwingi viungo na hata washambuliaji wake walikuwa wakilinda lango badala ya kushambulia kutokana na kasi ya Yanga hivyo kupoteza lengo la kupata ushindi mapema.
“Kama tungetangulia kupata bao mambo yangekuwa mazuri lakini muda mwingi wachezaji wangu walikuwa wakilinda lango kutokana na Yanga walivyokuwa wanashambulia.
“Mchezo huu wa kulinda ungekuwa mzuri kwetu endapo tungekuwa tunaongoza angalau kwa bao moja, sasa tulikuwa nyuma kwa bao moja muda mrefu halafu bado tukawa tunalinda lango, hapo unaona jinsi gani kwamba hata wachezaji wenyewe walikuwa bado na tatizo la saikolojia kwa kudhani Yanga inaweza kuwafunga mabao mengi zaidi,” anasema Liewig.
UBINGWA WA YANGA;
Tofauti na mechi nyingine za watani wa jadi zinavyokuwa, mara nyingi Simba na Yanga hukutana katika mechi za mwisho tena kwa kuwania pointi muhimu lakini katika mechi ya wikiendi iliyopita, mambo yalikuwa tofauti na hata Liewig ameliona hilo.
“Yanga ilikuwa tayari bingwa, sisi tulikuwa na uhakika wa nafasi ya
tatu huku tukiwa hatuwezi kupata nafasi ya pili kwa vyovyote hata kama tungeshinda. Hii ina maana Yanga, ilicheza kwa kujiamini zaidi huku ikitaka ushindi tu ili iweze kupewa kombe kwa furaha.
“Sisi tulitaka kucheza kwa kuweka heshima mbele ya mashabiki wetu huku tukipingana na makelele ya kufungwa mabao mengi na Yanga. Hili lilikuwa tatizo dogo japokuwa lilionekana kubwa baadaye,” anasema Liewig.
ANAZUNGUMZIAJE MUSTAKABALI WAKE…………….?
Liewig ambaye alijiunga na Simba Januari mwaka huu, anasema baada ya kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Yanga huku akiwa na msimamo wa kuendelea kutowatumia wakongwe, hajui mustakabali wa kazi yake utakuaje.
Kocha huyo muda mfupi baada ya kutua Simba, alihakikisha kikosi
kinakuwa na nidhamu na mchezaji aliyeona anaharibu nidhamu kikosini alimtimua. Katika ‘timuatimua’ yake, Liewig aliwasimamisha wachezaji Haruna Moshi ‘Boban’, Amir Maftah, Juma Nyosso, Felix Sunzu, Mwinyi Kazimoto, Paul Ngalema na Abdallah Juma, lakini baadaye aliwasamehe Kazimoto na Sunzu.
Uamuzi huu wa Liewig uliigawa Simba kwani si mashabiki tu hata
viongozi wapo waliomuunga mkono na wengine walipinga uamuzi wake huo wa ‘kuwatimua’ kikosini kina Boban.
“Uamuzi huu ulikuwa mzuri kwa manufaa ya Simba na ni mapema kuona uzuri wa uamuzi wangu lakini baada ya muda mtaelewa kwa nini nilifanya vile. Bado nina imani na wachezaji vijana ninaowatumia na hata akija kocha mwingine mambo yatakuwa vizuri kwao,” anasema Liewig.
“Kila msimu unapoisha, viongozi wa timu huketi pamoja na kufanya tathmini yao sasa siwezi kukuambia kama majaliwa yangu yatakuaje ndani ya Simba lakini uongozi wenyewe ndiyo utakaojua nini cha kufanya mimi naheshimu mkataba wangu hapa,” anamaliza Liewig.
Akizungumza katika mahojiano maalum, Liewig raia wa Ufaransa aliuambia mtandao huu kwamba, kikosi chake kilicheza vizuri lakini Yanga walitumia vizuri nafasi walizopata.
“Tulicheza vizuri kuanzia mwanzo hadi mwisho wa mchezo tatizo nafasi tulizopata hatukuzitumia vizuri na badala yake wenzetu Yanga walicheza vizuri na kutumia nafasi walizopata,” anasema Liewig.
Kocha huyo hata hivyo alisema anaamini kikosi chake kinachoundwa na wachezaji wengi vijana na wale waliokuwa hawapati nafasi kikosi cha kwanza, bado kina nguvu ya kufanya vizuri msimu ujao wa ligi na hata katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati ‘Kombe la Kagame’.
Liewig alitaja mambo makubwa manne yaliyoikwaza timu yake na kuruhusu kufungwa mabao 2-0 na Yanga;
SAIKOLOJIA;
“Kabla ya kuingia uwanjani si wachezaji tu hata mashabiki wetu wengi walijua timu yetu itafungwa, sasa kazi kubwa ilikuwa kuwaweka sawa wachezaji wetu hasa vijana katika hali ya kuhakikisha tunashinda mechi hii.
“Wakati sisi tukiwaza hivyo, wenzetu Yanga walikuwa wana uhakika wa ushindi na mbaya zaidi walikuwa wanawaza kuibuka na ushindi wa mabao mengi zaidi wakidhani kikosi chetu ni dhaifu,” anasema Liewig.
Liewig anakiri kwamba, pamoja na yote hayo lakini benchi la ufundi la Simba lilijitahidi kuwaweka sawa kisaikolojia lakini timu zilipoingia uwanjani ni wazi Yanga ilikuwa vizuri kisaikolojia katika ushindi kuliko wao.
PENALTI YA MUDDE;
Simba ilipata penalti dakika ya 28 baada ya beki wa Yanga, Nadir
Haroub ‘Cannavaro’ kumuangusha ndani ya eneo la hatari aliyekuwa mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa. Penalti hiyo ilipigwa na Mussa Mudde raia wa Uganda, lakini alikosa.
“Hadi tunapata penalti, Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0, hivyo kama tungepata penalti ile matokeo yangekuwa sawa na kuhamsha morali yetu ya kuhakikisha tunapata matokeo mazuri.
“Siku zote anayepiga penalti huwapa mashabiki uhakika wa kupata kwa asilimia kubwa, lakini Mudde amekosa na lile halikuwa lengo lake japokuwa umakini wa hali ya juu ulitakiwa kuwepo,” anasema Liewig.
KULINDA LANGO;
Liewig anasema kwa muda mwingi viungo na hata washambuliaji wake walikuwa wakilinda lango badala ya kushambulia kutokana na kasi ya Yanga hivyo kupoteza lengo la kupata ushindi mapema.
“Kama tungetangulia kupata bao mambo yangekuwa mazuri lakini muda mwingi wachezaji wangu walikuwa wakilinda lango kutokana na Yanga walivyokuwa wanashambulia.
“Mchezo huu wa kulinda ungekuwa mzuri kwetu endapo tungekuwa tunaongoza angalau kwa bao moja, sasa tulikuwa nyuma kwa bao moja muda mrefu halafu bado tukawa tunalinda lango, hapo unaona jinsi gani kwamba hata wachezaji wenyewe walikuwa bado na tatizo la saikolojia kwa kudhani Yanga inaweza kuwafunga mabao mengi zaidi,” anasema Liewig.
UBINGWA WA YANGA;
Tofauti na mechi nyingine za watani wa jadi zinavyokuwa, mara nyingi Simba na Yanga hukutana katika mechi za mwisho tena kwa kuwania pointi muhimu lakini katika mechi ya wikiendi iliyopita, mambo yalikuwa tofauti na hata Liewig ameliona hilo.
“Yanga ilikuwa tayari bingwa, sisi tulikuwa na uhakika wa nafasi ya
tatu huku tukiwa hatuwezi kupata nafasi ya pili kwa vyovyote hata kama tungeshinda. Hii ina maana Yanga, ilicheza kwa kujiamini zaidi huku ikitaka ushindi tu ili iweze kupewa kombe kwa furaha.
“Sisi tulitaka kucheza kwa kuweka heshima mbele ya mashabiki wetu huku tukipingana na makelele ya kufungwa mabao mengi na Yanga. Hili lilikuwa tatizo dogo japokuwa lilionekana kubwa baadaye,” anasema Liewig.
ANAZUNGUMZIAJE MUSTAKABALI WAKE…………….?
Liewig ambaye alijiunga na Simba Januari mwaka huu, anasema baada ya kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Yanga huku akiwa na msimamo wa kuendelea kutowatumia wakongwe, hajui mustakabali wa kazi yake utakuaje.
Kocha huyo muda mfupi baada ya kutua Simba, alihakikisha kikosi
kinakuwa na nidhamu na mchezaji aliyeona anaharibu nidhamu kikosini alimtimua. Katika ‘timuatimua’ yake, Liewig aliwasimamisha wachezaji Haruna Moshi ‘Boban’, Amir Maftah, Juma Nyosso, Felix Sunzu, Mwinyi Kazimoto, Paul Ngalema na Abdallah Juma, lakini baadaye aliwasamehe Kazimoto na Sunzu.
Uamuzi huu wa Liewig uliigawa Simba kwani si mashabiki tu hata
viongozi wapo waliomuunga mkono na wengine walipinga uamuzi wake huo wa ‘kuwatimua’ kikosini kina Boban.
“Uamuzi huu ulikuwa mzuri kwa manufaa ya Simba na ni mapema kuona uzuri wa uamuzi wangu lakini baada ya muda mtaelewa kwa nini nilifanya vile. Bado nina imani na wachezaji vijana ninaowatumia na hata akija kocha mwingine mambo yatakuwa vizuri kwao,” anasema Liewig.
“Kila msimu unapoisha, viongozi wa timu huketi pamoja na kufanya tathmini yao sasa siwezi kukuambia kama majaliwa yangu yatakuaje ndani ya Simba lakini uongozi wenyewe ndiyo utakaojua nini cha kufanya mimi naheshimu mkataba wangu hapa,” anamaliza Liewig.
Monday, May 20, 2013
TASWA FC YAWAFUNGA MABONDIA MABAO 2:0
ibrahim'bigright akitoa maelezo kwa timu ya mabondia huku thomas mashali akisikiliza kwa makini kabla ya kuingia.
alphonce mchumia tumbo akiwa chini ya ulinzi wa mabaki wa taswa
majuto omari wa taswa na jimwili lake kashindwa kabisa kufurukuta kwa daudi muhunzi.majuto ndie aliefunga bao la pili la taswa.hapa kabla hajatulizwa kibondia.
NGASA ATAMBULISHWA RASMI YANGA
Katibu Mkuu wa klabu ya Young Africans Lawrence Mwalusako leo amemtambulisha rasmi kwa waandishi wa habari mchezaji Mrisho Ngasa ambaye amerejea katika klabu yake ya zamani kufuatia ku
Mrisho Ngasa akiongea na waandishi wa Habari leo makao makuu ya klabu ya Yanga baada y akutambulishwa rasmi leo
malizika kwa mkataba wake wa miaka miatatu (3) dhidi ya timu ya Azam FC.
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu Mwalusako amesema Ngasa amerejea katika timu yake, alikuwa mchezaji wetu kwa muda mrefu kabla ya kuhamia katika timu ya Azam FC ambako alitumikia mkataba wa miaka 3 uliomalizika mwisho mwa msimu huu.
Naye mwenyekiti wa mashindano wa klabu ya Yanga Abdallah Bin Kleb amesema anashukuru kwa Ngasa kuamua kurudi nyumbani, kwani amekuwa mchezaji anayejitolea kwa moyo wake wote katika timu zake zote alizokuwa akichezea hali iliyompelekea kuendelea kuwa katika kiwango cha hali ya juu.
Kwa kweli mimi binafsi nimefurahi kijana kurejea nyumbani, amerejea katika timu inayomjali, inamsikiliza alisema Bin Kleb huku akimalizia kwa kusema kuwa Ngasa ataitumikia Yanga kwa mkataba wa miaka 2.
Aidha Ngasa mwenyewe amewashakuru wapenzi, washabiki na wanachama wa klabu ya Yanga kuwa naye kwa nyakati zote, nilipohamia Azam walikua wakishangilia, nilipohamia Simba pia walikuwa wakinipa moyo na kunishangilia pia.
Nimeamua kurudi katika timu yanga ya zamani sababu ndio sehemu pekee wanaponisikiliza na kunithamini, timu niliyotoka pamoja na kucheza kwa moyo wangu wote bado viongozi wake hawakua na imani na mimi hicho ndo kilichonipelekea kurudi katika timu yangu ya Yanga.
Ngsa anakua mchezaji wa kwanza kusajiliwa na klabu ya Yanga kwa ajili ya kuongeza nguvu katika kikosi kitachoitumikia Yanga katika msimu ujao.
DAIMA MBELE NYUMA MWIKO (DMNM)
EVER FORWARD BACKWARD NEVER (EFBN)
Mrisho Ngasa akikabidhiwa jezi ya klabu ya Yanga na katibu mkuu Lawrence Mwalusako
Source: www.youngafricans.co.tz
Sunday, May 19, 2013
HAWA NDIO WASHINDI WA DROO YA WESTERN UNION
![]() |
| Add caption |
Ligi ya vijana Dar kuanza Julai 29
KAMATI ya Ufundi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), kimetangaza kuanza kwa Ligi ya vijana walio chini ya umri wa miaka 15, itakayoanza Julai 29 mwaka huu.
Mkurugenzi wa Ufundi wa DRFA, Joseph Kanakamfumu, alisema jana baada ya kikao cha kamati hiyo, kilichokutana jana (Jumapili) kwenye Ukumbi wa Harbours Club Kurasini kuwa ligi hiyo ni moja ya mikakati ya chama hicho katika kuhakikisha mkoa wa Dar es Salaam unaibua vipaji kwa faida ya mkoa na Taifa.
Ligi hiyo itakuwa na faida kubwa kutokana na kuenda sawa na umri unaotumika na mashindano ya vijana ya Copa Coca Cola, ambayo mwaka huu yameanza kwa kushirikisha umri wa miaka 15.
Pia alisema ligi ya wanawake itaanza Agosti mwaka huu huku akiomba wadhamini nao kujitokeza kusaidia ligi hizo.
Wakati huo huo fomu kwa ajili ya kozi ya waamuzi na ile ya mpira wa miguu kwa ngazi ya cheti cha pili (Inter-Mediate) na zinapatikana kwenye ofisi za vyama vya mpira vya wilaya vya IDFA, KIFA na TEFA.
Mkurugenzi wa Ufundi wa DRFA, Joseph Kanakamfumu, alisema jana baada ya kikao cha kamati hiyo, kilichokutana jana (Jumapili) kwenye Ukumbi wa Harbours Club Kurasini kuwa ligi hiyo ni moja ya mikakati ya chama hicho katika kuhakikisha mkoa wa Dar es Salaam unaibua vipaji kwa faida ya mkoa na Taifa.
Ligi hiyo itakuwa na faida kubwa kutokana na kuenda sawa na umri unaotumika na mashindano ya vijana ya Copa Coca Cola, ambayo mwaka huu yameanza kwa kushirikisha umri wa miaka 15.
Pia alisema ligi ya wanawake itaanza Agosti mwaka huu huku akiomba wadhamini nao kujitokeza kusaidia ligi hizo.
Wakati huo huo fomu kwa ajili ya kozi ya waamuzi na ile ya mpira wa miguu kwa ngazi ya cheti cha pili (Inter-Mediate) na zinapatikana kwenye ofisi za vyama vya mpira vya wilaya vya IDFA, KIFA na TEFA.
PICHA ZA WAREMBO WA REDD'S MISS KIGAMBONI 2013
Warembo wanaoshiriki shindano la Redd's Miss Kigamboni wakiwa kwenye mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na kinyang'anyiro hicho kitakachofanyika Ijumaa Juni 7 mwaka huu kwenye ukumbi wa Navy Beach ulioko Kigamboni.
CPwaa ateuliwa kuwa msimamizi mkuu na MC wa michuano ya Foosball
PAMBANO LA SIMBA, YANGA LAINGIZA MIL 500/-
Pambalo la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.
Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.
Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.
Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
DAVID BECKHAM ALIVYOAGWA KWENYE MECHI YA MWISHO BAADA YA KUTANGAZA KUSTAAFU
Saturday, May 18, 2013
KWA STAILI YA AINA YAKE ROBERTO MANCINI AWAAGA MASHABIKI WA CITY
Siku moja ambayo gazeti la Daily Mail liliandika stori ya namna baadhi ya wachezaji wa walivyokuwa hawampendi kocha wao aliyefukuzwa Roberto Mancini, muitaliano huyo ambaye hakuachwa mpaka amalize mechi za ligi zimalizike alitumia ukurasa mzima wa gazeti la Manchester Evening kuweka tangazo la kuwaaga mashabiki liloandikwa "Manchester City supporters 3 UNFORGETTABLE YEARS," kwenye tangazo hilo pia kuna picha ya Mancini akiaaga huku kukiwa kuna makombe matatu ya EPL, FA na Ngao ya Hisani. Pia akaandika "You will always be in my heart. Ciao. Roberto Mancini."
Mancini alikuwa akipendwa na mashabiki hata baada ya kumaliza nafasi ya pili nyuma ya Man United na kufungwa na Wigan kwenye fainali ya FA Cup. Ingawa hali ilikuwa tofauti kwa wachezaji na wamiliki ambao wote walipoteza imani nae.
MPAMBANO WA SIMBA NA YANGA KATIKA PICHA.
Haruna Shamte akipambana na Simon Msuva wa Yanga...
Nahodha wa Yanga Nadir Haroub akinyanyua ubingwa wa ligi kuu ya VODACOM msimu wa 2012/2013
kikosi cha Simba kilichoanza hii leo....
Makocha wa Yanga Ernst Brandts pamoja na Felix Minziro wakijadiliana jambo.....
Sir Juma Nature pia alikuwepo kutoa burudani.....
Hili ndo lilikuwa bao la kwanza la Yanga lilifungwa na Didier Kavumbagu kwa kichwa....
Mrisho Ngassa akiwa amevalishwa jezi ya YANGA kwa mara nyingine tena huku akiwa amefurahi kweli kweli...
Mwamuzi wa mchezo wa leo Saanya akiwa chini mara baada ya kuumia.....
Subscribe to:
Posts (Atom)

























