Search This Blog

Loading...

Tuesday, June 18, 2013

NIGERIA YABAKI KUWA TIMU PEKEE KUTOFUNGWA KWENYE KOMBE LA MABARA TANGU KUANZISHWA KWAKE BAADA YA KUIPA KIPIGO CHA 6-1 TAHITI

 Timu ya taifa ya Nigeria jana usiku iliitandika TAHITI mabao 6-1 kwenye michuano ya kombe la mabara inayoendelea huko nchini Brazil. Mchezo huo umetengeneza takwimu nyingi sana - zipo kama ifuatavyo:

- Nnamdi Oduamadi ndi mwanasoka wa kwanza wa kiafrika kufunga mabao 3 kwenye mechi moja katika michuano ya Mabara 

 - Jonathan Tehau ndio mchezaji wa kwanza wa Tahiti kwenye michuano ya FIFA 


 - Nigeria wanabaki kuwa ndio timu pekee ambayo haijawahi kupoteza mchezo katika historia michuano hii kwa timu ambazo zimewahi kushiriki. Wakishinda mara mbili na kutoa suluhu mara mbili. 


 - Jonathan Tehau ndio mchezaji wa kwanza kufunga kwa pande zote kwenye mechi ya michuano ya FIFA - na bado timuyake ikafungwa. Wachezaji sita wengine waliowahi kufanya hivyo wote timu zao walizokuwa wakizichezea zilishinda mechi zao. 


 - Matokeo ya Tahiti 1-6 Nigeria ni matokeo ya moja kati ya mechi 8 za kombe la mabara zilizozaa magoli mengi - 7.  Ni mechi moja tu ya Brazil 8-2 Saudi Arabia ndio imezidi idadi hiyo ya mabao kwa mechi. 

HUYU NDIO MCHEZAJI MWENYE UMRI MKUBWA ZAIDI KUWAHI KUCHEZA KWENYE KOMBE LA MABARA - ANATOKA AFRIKA

Siku kama ya leo 2005
Golikipa wa Tunisia Ali Boumnijel alicheza kwenye mechi dhidi ya Ujerumani kwenye mashindano ya kombe la mabara akiwa na miaka 39 na miezi miwili, na akaweka rekodi ya mchezaji mwenye umri mkubwa kabisa kushiriki kwenye michuano hiyo.

SIKU KAMA YA LEO MWAKA 2009: EGYPT YAWEKA REKODI YA KUWA TIMU YA KWANZA KUIFUNGA ITALIA

Siku kama ya leo mwaka 2009
Mechi kati ya Italy na Egypt ilikuwa ni ya 100 kuchezwa kwenye historia ya kombe la mabara. Egypt waliifunga Italia kwa 1-0, na hivyo kuwa timu ya kwanza kutoka Africa kuifunga Azzurri.

THIAGO ALCANTARA APIGA HAT TRICK NA KUIPA SPAIN UBINGWA WA EURO (U21) KWA USHINDI WA MABAO 4-2 DHIDI YA ITALIA


Spain vs Italy 4:2 GOALS HIGHLIGHTS (U21 EURO... by footballdaily1

SAKATA LA USAJILI WA CRISTIANO RONALDO - REAL MADRID WAPO TAYARI KUMLIPA FEDHA ANAYOTAKA - TATIZO LABAKI KWENYE HAKI ZA TASWIRA YAKE.

Cristiano Ronaldo anakaribia kukubaliana na Real Madrid juu ya mkataba mpya wa kuendelea kubaki Santiago Bernabeu - kwa klabu hiyo ya jiji la Madrid kumfanya Ronaldo kuwa mchezaji anayelipwa fedha nyingi kuliko wote kwenye ulimwengu wa soka duniani.

Madrid wapo kwenye mazungumzo ya mwisho mwisho na wawakilishi wa Ronaldo kwa dili lenye thamani ya €155 million kwa mkataba wa miaka mitano - mkataba ambalo utamfanya Ronaldo aweke kibindoni €15m kwa mwaka baada ya kukatwa kodi - dili ambalo linatajwa kuwa la thamani zaidi katika historia ya soka duniani.

Ronaldo, ambaye amefunga mabao 201 katika 199 ndani ya misimu minne aliyokaa Santiago Bernabeu, aliwapa tumbo joto viongozi wa Madrid baada ya alhamisi ya wiki iliyopita kuandika kwenye mtandao wa Twitter kwamba: "All the news about my renewal with Real Madrid are false."


Ronaldo ambaye miezi kadhaa huko nyuma aliwahi kukaririwa akisema hana furaha ndani ya Madrid katika kile alichosema kwamba ni sababu zinazomfanya asiwe na furaha ndani ya klabu hiyo viongozi wa Madrid wanazifahamu- sababu ambazo inasemekana zimetokana na sapoti ndogo anayopata kutoka kwa klabu yake hasa katika mbio za kugombea Ballon d'Or, pia kitu kingine ni ugomvi wake na mchezaji mwenzie  Marcelo.

Madrid walimsajili Ronaldo kutoka Manchester United kwa rekodi ya uhamisho ya €94 million wakati wa kiangazi mnamo mwaka 2009, mara tu baada ya kurudi kwenye uongozi kwa Raisi  Florentino Perez. Kwa sasa Ronaldo analipwa kiasi cha €10m baada ya kodi.

Wakati Ronaldo aalipowasili Spain, kulikuwa na kitu kinachoitwa 'Beckham Law', ambayo iliwaruhusu wageni ambao wameishi nchini humo kwa miaka chini ya 10 na ambao wanavuna zaidi ya kiasi cha €120,000  kwa mwaka kulipa kodi ya chini kiasi cha asilimia 23 na sio ile ya kawaida ya asilimia 45, bado ilikuwepo. David Beckham alikuwa mmoja wa watu wa kwanza  kupata faida ya sheria hiyo baada ya kuhamia Madrid akitokea kupata  Manchester United mnamo mwaka 2003.

Japokuwa baadae serikali ya Spain ikaifuta sheria hiyo na sasa mkataba mpya wa Ronaldo utakuwa unakatwa kiasi cha 52% kama kodi. Hivyo, Madrid itabidi watoe package ya €31m ili baada ya makato Ronaldo abaki na kiasi cha €15m ambacho anakitaka.

Madrid, wanatambua umuhimu wa kuendelea kuwa na Ronaldo. Klabu hiyo hivi karibuni imemkosa Neymar, wakati wakionekana kukata tamaa ya uwapata wachezaji wa Dortmund Ilkay Gundogan na Robert Lewandowski. Wachezaji wengine ambao walikuwa kwenye hesabu zao kama vile Sergio Aguero na Radamel Falcao, hawatoenda Madrid pia, wakati Gareth Bale ni gharama zaidi kumpata na hataki kuomba uhamisho kutoka Tottenham na huku Edinson Cavani anaonekana kuwa hana thamani ya fedha ambayo Napoli wanaitaka kutokana mauzo ya Cavani. Hivyo kubaki na Ronaldo ni jambo muhimu.

Raisi wa klabu hiyo alikaririwa hivi karibuni akisema kwamba atafanya chochote kuhakikisha Mreno huyo anabakia ndani ya jiji la Madrid hata kumfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi kwenye ulimwengu wa soka.

Madrid sasa wapo tayari kumpa Ronaldo anachokitaka na kumfanya apate fedha nyingi kuliko Lionel Messi, ambaye analipwa kiasi cha €13m kwa mwaka kabla ya bonasi ndani ya Barcelona, na Falcao, ambaye anapata kiasi cha €14m kwa mwaka ndani ya Monaco. Samuel Eto'o analipwa kiasi cha €20m kwa mwaka na Anzhi Makhachkala, ingawa dili hilo la mcameroon huyo lina muda wa miaka mitatu tu na kwa ujumla dili la Ronaldo litampita Eto'o.

Tatizo kubwa na kizingiti kikubwa katika makubaliano ya mkataba mpya wa Ronaldo na Madrid ni suala la haki za taswira yake. Cristiano kwa sasa anamiliki asilimia 60 wakati klabu inachukua 40 zinazobakia. Ronaldo anahitaji maboresho makubwa kwenye suala hili - inaaminika anataka haki zake zote za taswira yake kwa maana ya asilimia 100 - kitu ambacho Madrid hawakubaliani nacho. Hapo ndipo makubaliano juu ya mkataba mpya yanapochelewa.

TIMU YA THAILAND YASAKA WACHEZAJI TANZANIA - GOSAGE MTUMWA APEWA ITC KWENDA KUCHEZA YEMENI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Mtanzania Gossage Mtumwa ili aweze kucheza mpira nchini Yemen.

Mtumwa ambaye anatoka katika kituo cha kukuza na kuendeleza vipaji cha Rollingstone cha Arusha aliombewa hati hiyo na Chama cha Mpira wa Miguu cha Yemen (YFA) kwa ajili ya kucheza nchini humo.

TFF inamtakia kila la kheri Mtumwa katika safari yake ya Yemen, na ni matarajio yetu kuwa atakuwa balozi mzuri wa Tanzania nchini humo ili wachezaji wengine wa Tanzania nao wapate fursa ya kucheza mpira wa miguu nchini Yemen.

KLABU THAILAND YASAKA WACHEZAJI TANZANIA
Klabu ya Thai Port Football ya Thailand inatafuta wachezaji nchini Tanzania kwa ajili ya kucheza mpira wa miguu nchini humo na katika nchi nyingine barani Ulaya.

Kupitia kwa wakala wake, klabu hiyo imetuma taarifa kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikitaka wachezaji wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 28 kwa ajili ya kuwafanyia majaribio ambapo watakaofuzu watacheza nchini humo na katika klabu nyingine za Ulaya ambazo wana ushirikiano nazo.

Wachezaji wenye nia ya kufanya majaribio wanatakiwa kutuma taarifa za wasifu wao (CV) kwa klabu hiyo kwa njia ya emaili, wawe na pasi ya kusafiria pamoja na pasi ya mchezaji (player passport).

Wakala atapitia vitu hivyo, na kwa wachezaji atakaowahitaji atawatumia tiketi za ndege na viza kwa ajili ya kwenda kufanya majaribio nchini humo, na watakaofanikiwa kabla ya kusaini nao mikataba watawasiliana na klabu zao nchini (kwa wale wenye klabu).

NSAJIGWA, BEN MWALALA NA WACHEZAJI WENGINE KUMALIZA KOZI YA UKOCHA JUMANNE

Nahodha wa zamani wa Yanga Shedrack Nsajigwa akiwa na Baadhi ya makocha wakiwemo wachezaji wa zamani wakifuatilia mafunzo ya ukocha ngazi ya pili.

Kocha mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage akitoa somo kwa makocha wanashiriki kozi ya ukocha ngazi ya pili ndani ya darasa kwenye Ukumbi wa Harbours Club, Kurasini.

Kocha mkuu wa Twiga Stars akitoa somo kwa makocha wa kozi ya ngazi ya pili kwa vitendo
KOZI ya makocha wa ngazi ya pili (Intermediate) inayosimamiwa na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), inatarajiwa kufungwa Jumanne ijayo baada ya kudumu kwa wiki nne.
Kozi hiyo ilianza Juni 3 mwaka huu kwenye Ukumbi wa Harbours Club, uliopo Kurasini chini ya Mkufunzi Rogasin Kaijage, ambaye ni Kocha wa timu ya Taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’ ambapo makocha mbalimbali pamoja na wachezaji wa zamani wamejitokeza kushiriki.
Ofisa Habari wa DRFA, Mohamed Mharizo alisema kozi hiyo imekuwa na mafanikio na wanatarajia makocha walioshiriki katika kozi hiyo watakuwa na mchango mkubwa katika kuendeleza mpira wa miguu katika mkoa wa Dar es Salaan na Taifa kwa ujumla.
“Hadi sasa tunashukuru kuona tunafanikisha kozi hii ambayo wengi wameitikia wito, mwisho wa kozi hii ndio mwanzo wa kozi nyingine.
“Lakini haya ya kozi ya makocha ni moja ya majukumu ya Kamati ya Ufundi ya DRFA yaliyoainishwa katika Katiba, hivyo hili ni moja ya shabaha yetu na mengine mengi mazuri yanafuata,” alisema Mharizo.
 Kozi hiyo ni ya kwanza kuendeshwa na DRFA tangu kuingia madarakani kwa uongozi mpya wa chama hicho Desemba 12, chini ya Mwenyekiti wake Almas Kassongo.

SUNDERLAND NA SYMBION KUJENGA ACADEMY MBILI ZA SOKA DAR ES SALAAM


CEO wa klabu ya Sunderland, Margaret Byrne, ameusifia ushirikiano na Tanzania kwamba ni hatua kubwa kuendelea mbele.
The Black Cats wameingia mkataba na kampuni ya nishati ya Power kujenga cademy kubwa ya soka nchini, ndani ya jiji la Dar es Salaam.
Raisi Jakaya Kikwete alitembelea makao makuu ya klabu ya Sunderland huko Wearside siku ya jumapili katika kukata rasmi utepe wa kuanza kwa project hiyo.
“Ni siku muhimu kwa klabu na klabu na mji wetu,” Byrne alisema.
“Kutembelewa na mheshimiwa Raisi hapa wakati akiwa UK kuhudhuria mkutano wa viongozi wa G8 ni jambo kubwa kutoka kwake na mawaziri wake. Ni zuri sana kwetu.
Hatua za mwanzo kwa ajili ya Academy zilizinduliwa siku hiyo ya jumapili, kwenye tukio ambalo lilihudhuriwa na mwenyekiti wa Sunderland Ellis Short.
Project hiyo itaisaidia Tanzania katika kukuza soka lake pia kuwapa nafasi kubwa vijana wadogo kabisa kuweza kuendeleza vipaji vyao kwenye academy hiyo. 
Sunderland watajenga majengo pamoja na kutoa makocha wa kufundisha.
“Hatua ya kwanza itatuhusisha sisi kufanya kazi na Symbion Power kujenga academy ya kijamii, tukiruhusu watoto wengi kuja na kufurahia kucheza mchezo wa soka,” Byrne alielezea.
“Hatua ya pili itatuhusisha sisi kufanya kazi na Symbion labda ikiwezekana na taasisi nyingine kujenga kituo cha kisasa cha kufundishia soka.
“Tutoa usaidizi mkubwa wa vifaa vingi tunavyotumia kwenye academy yetu ya Academy of Light na pia na maarifa tuliyoyapata na tunayoyapata kutoka kwenye project ya EPPP (Elite Player Performance Plan).


Monday, June 17, 2013

NIGERIA YAANZA NA BALAA KOMBE LA MABARA - WAIKANDAMIZA 6-1 TAHITI


Nigeria vs TahitI 6:1 GOALS HIGHLIGHTS by footballdaily1

MAGOLI YA SIKU: JUMA KASEJA NA CASILLAS NA MIKWAJU YA FAULO YA YAYA TOURE NA LUIS SUAREZ

IKER CASILLAS VS LUIS SUAREZ JUMA KASEJA VS YAYA TOURE

TAIFA STARS NA IVORY COAST WAINGIZA MILLIONI 500

Mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kundi C, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Ivory Coast (The Elephants) iliyochezwa jana (Juni 16 mwaka huu) imeingiza sh. 502,131,000 kutokana na watazamaji 57,203.

Tiketi za kushuhudia mechi hiyo ziliuzwa kwa sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.

Mgawanyo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ni sh. 76,596,254.24 wakati wa gharama za uchapaji tiketi ni sh. 7,809,104.

Asilimia 15 ya uwanja sh. 62,658,846.26, asilimia 20 ya gharama za mechi sh. 83,545,128.35 na asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 20,886,282.09.

Asilimia 60 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 250,635,385.06 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 12,531,769.25 ambayo ni asilimia 5 kutoka kwenye mgawo wa TFF.

Mechi iliyopita ya Stars dhidi ya Morocco (Lions of the Atlas) kwenye uwanja huo iliingiza sh. 226,546,000.

BAADA YA KUIKOSA SAFARI YA BRAZIL 2014 - TAIFA STARS SASA KUINGIA KAMBINI JULAI 4 - SAMATTA NA ULIMWENGU WATEMWA

Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen ameiita tena kambini timu hiyo Julai 4 mwaka huu kujiandaa kwa mechi ya kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inavunja kambi leo (Juni 17 mwaka huu) baada ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, kundi C Kanda ya Africa dhidi ya Ivory Coast iliyochezwa jana (Juni 16 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kim amesema wachezaji watakaoitwa kambin ni wote walioko kwenye timu hivi sasa isipokuwa Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaocheza mpira nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) katika klabu ya TP Mazembe Englebert.

Wachezaji hao ni Juma Kaseja, Aishi Manula, Aggrey Morris, Mwadini Ally, Ally Mustafa, Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Erasto Nyoni, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd, Haruni Chanongo na Zahoro Pazi.

Mechi hiyo namba 37 dhidi ya Uganda (The Cranes) itachezwa jijini Dar es Salaa kati ya Julai 12 na 14 mwaka huu wakati ile ya marudiano itafanyika wiki mbili baadaye katika Uwanja wa Mandela ulioko Namboole nje kidogo ya Jiji la Kampala.

RAISI JAKAYA KIKWETE ATEMBELEA KLABU YA SUNDERLAND YA UINGEREZA






SUALA LA TANZANIA KUTOKUWA NA UWEZO WA KWENDA BRAZIL 2014 LILIKUWA DHAHIRI TANGU MWAKA 2011.

Jumapili ya jana matumaini ya watanzania kuishuhudia timu yetu ya taifa ikicheza michuano ya Kombe la dunia yaliisha rasmi baada ya kupoteza mchezo muhimu dhidi ya Ivory Coast kwa kufungwa 4-2 katika uwanja wa Taifa.
Kiuhalisi watu wengi walianza kupoteza matumaini baada ya kufungwa wiki iliyopita jijini Marrakech 2-1 na Morocco, lakini mimi kama Shaffih Dauda nilishauona uhalisia wa nafasi ya Tanzania kwenda Brazil kwamba ni finyu mno. Hili nililiona tangu mwanzo wakati inajiandaa kuanza kuisaka tiketi ya kwenda Brazil.

Ilikuwa tarehe 9 November, 2011 Siku ya jumatano niliandika makala yaliyokuwa na kichwa cha habari "WATANZANIA TUSAHAU WORLD CUP 2014."
  


Niliyoyandika takribani miaka mwili iliyopita yamejidhihirisha jana. Nguvu iliyotumika katika kuhakikisha Stars inacheza World Cup 2014 ihamie katika kuunda mfumo mzuri wa soka letu ambao ndio mkombozi  pekee katika kuifanya Tanzania kung'ara katika soka la kimataifa. Zile kamati za saidie stars ishinde ziundwe sasa au iliyopo iendelee kwa malengo ya kuhakikisha tunajipanga vizuri ili mnamo tutakapoanza safari ya kuitafuta nafasi ya kwenda Russia 2018 tunakuwa tayari kiushindani ili kuweza kupambana na timu yoyote tutakayopangwa na hatimaye tutimize ndoto yetu ya kushiriki michuano mikubwa zaidi kwenye ulimwengu wa soka.

Sunday, June 16, 2013

UCHAMBUZI MCHEZO WA TANZANIA VS IVORY COAST - ILIKUWA LAZIMA IVORY COAST ISHINDE NDANI NA NJE YA UWANJA



TIMU ya soka ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars imefungwa mabao 4-2 dhidi ya Ivory Coast na kuzima harakati zake za kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia 2014 huko Brazil.
Watanzania wengi na wadau wa michezo walidhani Taifa Stars ingeweza kusonga mbele katika harakati hizo za kufuzu kucheza Kombe la Dunia 2014, lakini sasa ukweli umejidhihirisha.
Sasa wengi wamekubaliana na uhalisia wa mambo kwamba, inahitaji muda kidogo kuona Taifa Stars ikisonga mbele katika kuelekea kufuzu Kombe la Dunia na siyo rahisi kama ilivyodhaniwa hapo kabla.
Ni mambo mengi yaliyotokea katika mchezo dhidi ya Ivory Coast ambayo yaliigharimu Taifa Stars licha ya uwanja kujaa idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa wakiishangilia timu yao bila kuchoka.
Jambo la msingi ni kwamba, Taifa Stars ikiwa katika harakati za kuhakikisha inafuzu Kombe la Dunia wengi tulisahau kwamba, kwa ‘reality’ ilikuwa ngumu kwa Taifa Stars kufuzu fainali hizo japokuwa kwa mapenzi tulidhani timu hii ingeweza kufuzu kwa kuanza na vipigo kwa timu za Morocco na Ivory Coast.
Tukitazama mchezo kati ya Taifa Stars na Ivory Coast kuna baadhi ya mambo yalionekana kwamba bado tuna safari ndefu ya kufuzu Kombe la Dunia kama kweli tuna nia ya kufanya hivyo.
Mambo mengi mno yalijitokeza katika mchezo kati ya Taifa Stars dhidi ya Ivory Coast na haya ni machache kati ya mengi yake;

TAIFA STARS ILICHEZA KUFURAHISHA MASHABIKI SIYO KUIFUNGA IVORY COAST
Kiungo wa Manchester City, Yaya Toure alicheza kama mshambuliaji na alitimiza majukumu yake kama straika hasa kwa kutokubali kukaa na mpira kwa muda mrefu licha ya kuwa na uwezo wa kufanya hivyo.
Wakati Toure mwenye uwezo wa kumiliki mpira atakavyo na kufanya jambo lolote hakutoa nafasi hiyo zaidi ya kutafuta ushindi kwa timu yake, viungo na wachezaji wengi wa Taifa Stars walikuwa wakitumia muda mwingi kukaa na mpira bila ya sababu ya msingi.
Kiungo Salum Aboubakar ‘Sure Boy’ mara nyingi alikuwa kitumia muda mwingi kukaa na mpira na kutaka kupambana na wachezaji wa Ivory Coast licha ya kuonekana wazi kwamba mara zote alizidiwa nguvu.
Tazama hata Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto na Frank Domayo walikuwa wakitumia muda mwingi ‘ku-hold’ mipira huku wakitoa pasi zisizo na macho na kujikuta wakipoteza mipira mingi kutokana tu na vitendo vyao vya kuchelewesha mipira.
Pamoja na vitendo hivyo kuwa hatari kwa timu, lakini mashabiki walikuwa wakiwashangilia kwa nguvu viungo wa Taifa Stars bila ya kujua madhara ya kufanya hivyo. Hao walijali zaidi kushangiliwa kuliko umuhimu wa mchezo husika.
Taifa Stars ilihitaji zaidi kucheza kwa kutokubali kukaa na mpira kwa muda mrefu kwa wachezaji wake ili kuitengeneza nafasi za haraka za kupata bao ili iweze kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.
Kuanzia Sure Boy, Kiemba, Kazimoto na Domayo, wote walionekana kufurahishwa na kelele za mashabiki waliokuwa wakiwashangilia kutokana na chenga na madoido mengine waliyokuwa wakiyafanya uwanjani.

SAFU YA ULINZI ILIPAPARIKA
Ilikuwa kama kila mchezaji ameahidiwa kiasi kikubwa cha fedha, kwani mara nyingi wachezaji wa Taifa Stars hawakucheza katika nafasi zao na hilo liligharimu timu na kujikuta wakilala mabao 4-2.
Erasto Nyoni ndiye beki anayeweza kuondoka na lawama nyingi lakini halikuwa kosa lake wakati mwingine kwani alilazimika kwenda katikati kusahihisha makosa ya mabeki wa kati na kuisahau nafasi yake.
Ilionekana wazi kwamba yalikuwepo mawasiliano hafifu juu ya kutengeneza mtego wa kuotea yaani ‘offside trick’ na matokeo yake Ivory Coast walitumia vyema mwanya huo na kujipatia mabao manne.
Baada ya kuonekana ‘njia’ tangu dakika za mwanzo, beki Erasto Nyoni inaonekana hakupata ushauri wa kutosha kuhusu kutulia na kucheza soka kwani hata makelele ya mashabiki yalimfanya aonekane mtu asiyefaa kikosini. Lakini alikuwepo benchi anayeweza kumudu nafasi yake moja kwa moja?

NGUVU HAFIFU
Wachezaji wengi wa Taifa Stars walionekana kutokuwa na nguvu ya kupambana na wenzao wa Ivory Coast kutokana na hali halisi ya miili yao.
Sure Boy mfupi na mwenye mwili mdogo alionekana kama mchezaji wa kawaida mbele ya Yaya Toure mwenye mwili mkubwa na nguvu, na mara nyingi Toure aliiwahi mipira ambayo ingeweza kuwahiwa na Sure Boy.
Domayo naye hakuweza kufua dafu mbele ya Traore Lucina na Jean Jacques ambao wote ni watu wa miraba minne. 
   
WAO WALIMKATAA KALOU, SISI TUKAFUATA SAMBUSA
Kabla hata ya mapumziko, waandishi kadhaa wa Ivory Coast walionekana kutopendezwa na uchezaji wa Salomon Kalou ambaye muda mwingi kila alipopewa mpira alikuwa akitaka kukaa nao kwa muda mrefu kama ilivyokuwa kwa kina Sure Boy na wengine wa Taifa Stars.
Waandishi hao walionekana wazi kuchukizwa na hali hiyo na mara kwa mara walionyesha wazi kutoridhika na uchezaji wa Kalou.
Ulipofika wakati wa mapumziko, waandishi hao walishuka chini katika vyumba vya kubadilishia na kuzungumza na baadhi ya maafisa wa timu yao ili kutazama uwezekano wa kumpumzisha Kalou kwa maslahi ya nchi.
Wakati hayo yakitokea kwa Ivory Coast, waandishi wa Tanzania walikuwa wamekaribishwa ukumbi wa VIP kupata vitafunwa kama sambusa, mishikaki na vinywaji baridi, hao hawakuwaza kupeleka mawazo yao kwa benchi la ufundi na hata wangefanya hivyo wasingesikilizwa kutokana na utaratibu ulivyo.
Mbaya zaidi siyo waandishi tu, hata viongozi kadhaa wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars nao walionekana wakiwa VIP wakijichana kana kwamba Taifa Stars ipo katika nafai nzuri. Kumbuka hadi muda huo timu ilikuwa ipo nyuma kwa mabao 3-2.
HONGERA ULIMWENGU
 
Kama kuna mchezaji wa Ivory Coast aliyeomba mpira uishe haraka kuliko wengine basi ni Bamba Souleman ambaye alikuwa akicheza kama beki wa kati anayemkaba mshambuliaji wa Taifa Stars, Thomas Ulimwengu.
Ulimwengu alimmudu vizuri Bamba kiasi cha kumkimbiza na kuufanya mpira atakavyo hadi kufunga bao moja. Mara nyingi Bamba alizidiwa nguvu na kasi na Ulimwengu kiasi cha kulalamikiwa na wenzake.
Kama wachezaji wanne tu wa Taifa Stars wangeweza kucheza kama Ulimwengu, ni wazi timu hiyo ingepata matokeo mazuri na ya kuridhisha.  

BY ELIUS KAMBILI

KALI YA LEO: HIVI NDIVYO TV YA UWANJA WA TAIFA ILIYOBUGI

Majina ya wachezaji na bendera ni Ivory Coast - Jina la timu ni Morroco. 

MJADALA: UNADHANI NINI KIFANYIKE KATIKA KUIBORESHA TAIFA STARS KUFANYA VIZURI MICHUANO YA KIMATAIFA???


Toa maoni yako kuhusu nini kifanyike katika kuiboresha timu ya Taifa ili iweze kufanya vizuri kwenye michuano ijayo ya kimataifa. Nini kifanyike tuweze kufuzu AFCON 2015 na Kombe La Dunia mwaka 2018???

PICHA ZA MCHEZO WA TANZANIA DHIDI YA IVORY COAST




 Kikosi cha timu ya soka ya Tanzania 'Taifa Stars'
Kikosi cha Ivory Coast.
 Waamuzi wa mechi ya Stars na Ivory Coast wakiwa katika picha ya pamoja na manahodha wa timu zote mbili. 
Benchi la ufundi la timu ya Taifa Stars. 
 Benchi la ufundi la timu ya Ivory Coast.
 Thomas Ulimwengu akimtoka mchezaji wa Ivory Coast, Bamba Souleman
 Ni hatari.
 Heka heka.
Gooooooooo. 

 Thomas Ulimwengu akishangilia bao la pili la Stars.
Mashabiki wakishangilia.
Wachezaji wa Taifa Stars wakishangilia bao la kwanza la timu hiyo katika mchezo wa kufuzu fainali za kombe la dunia dhidi ya Ivory Coast. Stars ilifungwa 4-2. 
 Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen akilalamikia penalti iliyotolewa na mwamuzi, Mehdi Abid.  
 Beki wa Taifa Stars, Shomari Kapombe akitafuta mbinu za kumtoka mchezaji wa Ivory Coast, Aurier Alain katika mchezo wa kufuzu fainali za kombe la dunia uliuofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Wachezaji wa Ivory Coast wakisalimia na wenzao.
Mshambuliaji wa Taifa Stars, Amri Kihemba akiwatoka mabeki wa timu ya Ivory Coast,  katika mchezo wa kufuzu fainali za kombe la dunia uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Ivory Coast ilishinda 4-2. 
Mshambuliaji wa Stars, Thomas Ulimwengu akimtoka, Bamba Souleman.
PICHA ZOTE KWA HISANI YA HABARIMSETO BLOG


JB, IRENE UWOYA, RAY WANG'ARA TUZO ZA BONGO MOVIEZ 2013


Mkurugenzi wa Kampuni ya Steps, Diresh Solanki akimpa tuzo msanii bora wa kiume katika tasnia ya filamu nchini Jacob Steven JB wakati wa utoaji wa tuzo hizo zilizofanyika usiku wa kuamkia leo na kuhudhuliwa na wasanii wengi nchini hii ni kwa mara ya kwanza steps inaandaa tuzo hizi zitakazokuwa zikitolewa kila mwaka.Picha nawww.burudan.blogspot.com
Pazia ra Tuzo za Steps Bongo Movie Awards ukiwa umefunguliwa na waziri wa Sayansi na Teknolojia Makame Mbawala


Mzee Majuto akipokea Tuzo ya msanii bora wa uchekeshaji


Msanii Steve Nyerere akipokea Tuzo

Msanii Nice Mohamedi 'Mtunis' akipokea tuzo ya Mwaka 2012 zilizoandaliwa kwa mara ya kwanza na kampuni ya Steps Entatainment tuzo hizi zitakazokuwa zikitolewa kila mwaka.Picha na www.burudan.blogspot.com

MAMA SHILOLE AKIWA JUKWAANI

Mtoto Jenifa akichukua tuzo yake

Riyama akipokea tuzo yake
Msanii Niva akichukua TUZO ya msanii bora Chipkizi kulia yupo msanii mwenzake Rado

Photo: Mjumbe wa Kamati ya saidia Taifa Stars Ishinde, Ridhiwani Kikwete kushoto akimkabidhi tuzo Haji Adamu kwa niaba ya Jimmy Mponda aliyeshinda msanii bora wa Filamu za Mapigano wakati wa utoaji wa tuzo hizo zilizofanyika kwa mara ya kwanza nchini na kuandalia na kampuni ya Steps Picha na www.burudan.blogspot.com

Mjumbe wa Kamati ya saidia Taifa Stars Ishinde, Ridhiwani Kikwete kushoto akimkabidhi tuzo Haji Adamu kwa niaba ya Jimmy Mponda aliyeshinda msanii bora wa Filamu za Mapigano wakati wa utoaji wa tuzo hizo zilizofanyika kwa mara ya kwanza nchini na kuandalia na kampuni ya Steps Picha na www.burudan.blogspot.com
Mjumbe wa Kamati ya saidia Taifa Stars Ishinde, Ridhiwani Kikwete wa tatu kushoto akiwapongeza baadhi ya wasanii wa marehemu Kanumba baada ya kuwakabizi tuzo

Mkurugenzi wa Kampuni ya Steps Dilesh Solanki akimkabizi tuzo ya mwongozaji bora wa filamu nchini kwa mwaka 2012 Vicent Kigosi 'Ray ' wakati wa utoaji wa tuzo hizo zilizofanyika usiku wa kuamkia jana usiku.  
Mkurugenzi wa Kampuni ya Steps Dilesh Solanki akifafanua jambo baada ya kumkabizi tuzo Vicent Kigos 'Ray' ya mwogozaji bora wa filamu nchini kwa mwaka 2012.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Steps wakipokea tuzo

Baadhi ya wasanii wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa tuzo zao za kwanza kwa mwaka 2012 zilizozaminiwa na kampuni ya steps.
MPIGA PICHA MOHAMED ARALAKIA ZA COVERS MBALIMBALI ZA KAMPUNI YA STEPS AKIPOKEA TUZO

:KAMPUNI ya Usambazaji wa filamu ya Steps Entatainment ya jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyopita ilitoa tuzo kwa wasanii bora waliofanya vizuri katika tasnia ya filamu nchini kwa mwaka 2012 ikiwa ni kwa mara ya kwanza kuanzishwa kwa tuzo hizo

Akizungumzia tuzo hizo Mkurugenzi wa Kampunu hiyo Direshi Solanki amesema kuwa tuzo hizo watakuwa wakizitoa kila mwaka kwa kuleta maendeleo ya filamu nchini kampuni hiyo iliyojikita katika kusambaza filamu za wasanii wameweka historia ya kuigwa kutokana na kuanzisha tuzo hizo

Baadhi ya washindi ambao waliopatikana katika tuzo hizo wa kwanza ni Steven Mangendela 'Steve Nyerere', Issa Mussa 'Cloud 112' Mohamed Nurdini 'Chek budi' Nice Mohamed 'Mtunisi' Irene Paul akinyakuwa msanii bora chipukizi wa kike

Wakati katika kinyanganyiro cha kumpata msanii bora wa kiume alinyakuwa Jacob Stevin 'JB' huku msanii bora wa kike ikienda kwa mwana dada Irene Uwoya, na msanii bora wa filamu za mapingano ilikwenda moja kwa moja kwa Jimmy Mponda 'Jimmy Masta'

Wakati katika kipengere cha muhongozaji bora wa filamu kilikwenda kwa vicent Kigosi' Ray' na kampuni yake ya RJ Filamu

Mbali na hivyo kulikuwa na tuzo za heshima kwa wasanii waliofanya vizuri lakini kwa sasa hawapo duniani moja ni kwa Stevin Kanumba,Saidi Kilowoko 'Sajuki' John Stefano, Hussein Ramadhani Mkiety 'Sharo Milionea'

Katika utoaji wa tuzo huzo kulikua na burudani nyingi zikiongozwa na Odama Bendi