Search This Blog

Loading...

Saturday, February 4, 2012

CHELSEA VS MAN UNITED: ANTONIO VALENCIA MCHEZAJI MWENYE FUNGUO YA USHINDI WA UNITED DHIDI YA CHELSEA



Manchester United wanakutana na Chelsea leo hii katika mchezo ambao unaweza ukawa moja ya ficture muhimu sana za msimu huu. United waliwafikia City kileleni katikati mwa wiki hii, hivyo watahitaji kuendelea na performance nzuri kama wanataka kujisogeza wenyewe kileleni katika nafasi ya kwanza.

Wakienda kwenye mechi, Chelsea itakuwa bila wachezaji weake muhimu wawili. Ashley Cole ana adhabu kutokana na kadi mbili za njano alizopata katika mchezo dhidi ya Swansea, na John Terry atakuwa nje kwa majeraha ya goti. Kwa hakika huu ni muda muafaka kwa United kuwaadhibu tena Chelsea.

Ama kwa hakika ukimtaja mchezaji ambaye yupo katika form nzuri kwa United msimu huu lazima atakuwa Antonio Valencia, na mechi hii dhidi ya Chelsea itakuwa nafasi kubwa kwake kuitawalana kujivalisha taji la Winga bora wa United msimu huu. Huku Ashley Cole nje, Valencia ana uwezekano mkubwa wa kucheza dhidi ya aidha bwana mdogo Ryan Bertrand au Jose Bosingwa aliye nje ya form, kati ya hawa wote wawili simuoni wa kumkabili in-form Valencia.

Ukweli ni kwamba wakati mashabiki wengi wakisema Micheal Carrick ndio the most underrated player katika kikosi cha United, mtu angestahili title hii ni Valencia  mpaka wiki chache zilizopita. Katika miezi michache iliyopita Valencia amethibitisha kwamba yeye ni moja ya wachezaji muhimu sana  katika United squad.

Wakati Nani akibaki kama mchezaji mwenye kipaji binafsi zaidi katika klabu, consistency ya Valencia ni balaa. Katika mechi 11 alizoanza za EPL msimu huu amefunga magoli mawili na kutoa assists 9.

Naweza hata nikasema kwa sasa Valencia ndio winga wa kulia mzuri kuliko wote katika premier league. Rivals wake wa karibu wanaweza kuwa Theo Walcott au Aaron Lennon, ambao kati yao hakuna aliyeonyesha mambo ya kutisha kama alivyofanya “Tony V” katika wiki chache zilizopita.

Wakati udhaifu dhahiri wa Valencia ni kushindwa kucheza na mguu wa kushoto, lakini hili jambo bado halijaonekana kuwa kikwazo kikubwa kipindi cha mechi kwani mara nyingi huwa anafanikiwa  kuurudisha mpira katika upande wake wa kulia na kutoa krosi nzuri na zenye madhara katika lango la adui.

Kwanini naamini Valencia atakuwa mwamuzi mkubwa wa mchezo huu? Well, kama nilivyosema mwanzoni watu watakaopewa jukumu la kumkaba ni aidha bwana mdogo ambaye hana uzoefu Ryan Bertrand au Bosingwa. La muhimu zaidi, uwezo wake wa kutoa pasi za mwisho na kumtoa mchezaji wa upinzani nje ya box utaendelea kuwa tishio kwa ukuta wa Chelsea uliodhaifu tena wakiwa wanamkosa Terry.

Huku mtu ambaye amekuwa akifanya makosa kila kukicha David Luiz akitegemewa kuanza pamoja na Gary Cahill, uwezo wa Valencia unaweza ukazua balaa katika final third ya Chelsea. Krosi za Valencia ni hatari zaidi, na kuwa-pair Luiz na Cahill linaweza kuwa tatizo jingine la kushughulika nalo.

Huku Young akiwa anarudi kutoka katika majeruhi, inabidi ushangae ni vipi ataweza kurudisha namba yake kwa form hii aliyonayo “Tony V”. Valencia ni mchezaji ambaye kwa sasa ni muhimu zaidi katika kikosi cha United, na ataendela kuwa hivyo katika mchezo dhidi ya Chelsea leo Jumapili. Tegemea magoli.
NAWASILISHA.

CHELESA VS MAN UNITED: MAMBO MANNE YA KIUFUNDI AMBAYO VILLAS-BOAS AKIFANYA YATAINUFAISHA CHELSEA DHIDI YA UNITED



Hapo zamani kidogo Chelsea waliweka rekodi ya kutofungwa katika mechi 86 walizocheza katika uwanja wao wa Stamford Bridge.
Ingawa sasa mambo ni tofauti, vipigo vya hivi karibuni dhidi ya Aston Villa, Liverpool na Arsenal vimebadili mtazamo wa kiwanja hicho maarufu kama darajani “Darajani”.
Hiki ni kitu ambacho Sir Alex Ferguson wa Manchester United atakitumia katika mchezo wa jumapili kwa sababu timu yake ina rekdi nzuri ya ugenini kuliko timu zote katika ligi msimu huu.
Haya mambo manne ya kiufundi ambayo Villas-Boas anapaswa kufanya ili kuweza kuwakalisha United darajani.


RYAN BERTRAND AANZE BADALA YA BOSINGWA KATIKA NAFASI YA BEKI WA KUSHOTO.
Ashley Cole amekuwa akicheza chini ya kiwango mno msimu huu, lakini amekuwa akicheza kila siku kwa kuwa hakuna mbadala anayeweza kushindania nae namba.
Lakini sasa, Cole akiwa amesimamishwa, Andre Villas-Boas amepewa nafasi ya kukaa na kufikiri vizuri.
Nani aanze upande wa beki wa kushoto?
Kuna washindani wawili: Jose Bosingwa na Ryan Bertrand.
Vilaas-Boas ansingekuwa na wakati mgumu kama angelijumlisha jina Bertrand katika kikosi cha champions league. Kama angefanya hivyo, Bertrand angeanza dhidi ya Bayer Leverkusen, mchezo ambao Ashley Cole aliukosa kutokana na maumivu ya enka.
Badala yake, Villas-Boas alilazimika kuidhoofisha timu yake kwa kuamua kumuanzisha Bosingwa katika upande wa kushoto, jambo lilopelekea Gonzalo Castro kumtawala beki huyo wa kireno ambaye yupo nje ya form.

Sidhani kama ni jambo la sahihi kwa Bosingwa kuanza katika mechi dhidi ya United  kwa naamini atakuwa anakimbiza kivuli cha mtu ambaye katika siku za hivi karibuni amekuwa moyo wa United dimbani Luis Antonio Valencia.

Pia kumtumia Bertrand in the deep end, manager wa Chelsea atapata majibu kwamba Bertrand ni mtu sahihi kumrithi Cole ndani ya kikosi cha Chelsea.

 LUKAKU APEWE MUDA WA KUCHEZA ZAIDI
Andre Villas Boas hakuwahi kumuhitaji Romelu Lukakau, kama ambavyo hakuwa akitaka kumsaini Kevin De Bruyne, na matokeo yake Portuguese manager ameiharibu confidence ya Lukaku, ambaye bado hajapewa nafasi zaidi.

Kwa wale ambao mnasema. “Oh bado hayupo tayari” – Kweli?
Akiwa na miaka 17, tayari ameshafunga magoli 39 na kutoa assists 14 katika michezo rasmi 95.

Nini walikuwa wanafanya Lionel Messi na Cristiano Ronaldo walipokuwa na miaka 17? Walikuwa ndio kwanza wanaonja ladha ya soka la kulipwa.

Lukaku ni mtoto aliyepevuka kikubwa zaidi na inakatisha tama kuona Villas-Boas ameshindwa kukiendeleza kipaji cha  mtoto huyu mwenye nguvu kama watu wazima.

Kuliko kumpa sub Paulo Ferreira, Villas-Boas anahitaji kumpa Lukaku muda zaidi kiwanjani kutoka atleast dakika 20-30, ikiwa Fernando Torres ataendlea kuzingua dhidi ya United.

3: JONNY EVANS
Nini ni udhaifu wa Jonny Evans? Tackling, kwa sababu ana maamuzi mabovu.

Mifano hai ni kama tackle aliyoifanya dhidi ya Stuart Holden, kumfanya Oscar Coldozo wa Benfica kuonekana kama hatari zaidi ya uwezo wake na kubwa zaidi alivyomvuta Mario Balotelli.
Hii ndio sababu kubwa inabidi Villas-Boas inabidi ampange Juan Mata katikati, kwa kuwa mhispania huyu na uwezo wake utamfanya Evans acheze ovyo na kusababisha madhara kwa United.
Evans ana wastani mzuri wa kupiga pasi, ana asilimia 89.7. hivyo ni mmoja kati centre backs walio salama zaidi duniani linapokuja suala la kusambaza mipira.

Villas-Boas anapaswa kumlazimisha Torres kumpa presha Evans kipindi beki huyo wa United anapokuwa na mpira.
Kwa kufanya hivyo, itamfanya Evans akose kujiamini na kushindwa kupiga pasi vizuri hivyo kufanya makosa ambayo yatainufaisha Chelsea.

4: KUPIGA MASHUTI YA MBALI IKIWA DE GEA ATAKAA LANGONI.

Huku Anders Lindegaard akiwa nje, David De Gea lazima atakuwa ni no.1, lakini hayupo katika form.

Chelsea watajidhoofisha wenyewe kwa kumuanzisha David Luiz na labda Jose Bosingwa, hivyo hata Manchester United watafanya hivyo kwa kumuanzisha De Gea katika milingoti mitatu.
Ni jambo la kushangaza kuona United walimnunua De Gea huku akiwa na matatizo ya macho.

Na ndio maana haishangazi kuona yeye ndiye aliekuwa golikipa aliyefungwa zaidi kwa mashuti ya mbali katika msiimu wa 2010-11 wa la liga. Hivyo Chelsea wanachotakiwa kufanya ni kupiga mashuti ya mbali kila wanapopata nafasi na hali hiyo itaongeza  presha kwa De Gea na mwishoanaweza kufanya makosa ambayo yatainufaisha Chelsea.

SIMBA YAGONGWA NA VILLA SQUAD VODACOM PREMIER LEAGUE


Klabu ya Simba ya Dar es Salaam leo imekubali kipigo kutoka kwa Villa SQUAD katika mfulululizo wa ngwe ya lala salama ya Vodacom Premier League.
Katika mchezo huo uliofanyika jijini DSM katika uwanja wa taifa Villa ilifanikiwa kuondoka na pointi 3 baada ya kuibuka na ushindi wa goli 1-0.
Villa ambao walimaliza mchezo huo wakiwa 10 dimbani walifunga goli lao katika dakika ya 40 likiwekwa kimiani na Nsa Job.
Katika hatua nyingine Coastal Union ya Tanga imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuifunga Moro United 1-0 katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa Chamazi – Dar es Salaam. Goli la Coastal lilitiwa kimiani na Rashid Yusuf katika kipindi cha pili.
Mashabiki wa Simba wakiwa hawaamini kilichotokea.

Matokeo mengine ya VPL Ruvu shooting wametoka sare pacha na Polisi Dodoma.


MSIMAMO WA VPL.
Kwenye Mabano Idadi ya Mechi Zilizochezwa.
1. Simba SC (16) 34
2. Yanga (15) 31
3. Azam FC (15) 29
4. JKT Oljoro (15) 26
5. Mtibwa Sugar (15) 22
6. Kagera Sugar (15) 20
7. Ruvu Shooting (16) 18
8. JKT Ruvu (15) 17
9. African Lyon (15) 17
10. Coastal Union (16) 17
11. Moro United (16) 15
12. Villa Squad (16) 13
13. Toto Africa (15) 13
14. Polisi Dodoma (16) 13



david luis alipomuombea Torres!

EXCLUSIVE INTERVIEW NA MICHAEL WAMBURA!

BOFYA HAPA CHINI UMSIKILIZE MICHAEL WAMBURA AKIZUNGUMZIA MIZENGWE YA SOKA LA BONGO.

BREAKING NEWS! ANGETILEH OSIAH AMELAZWA AGA KHAN HOSPITAL!

TAARIFA AMBAZO ZIMETUFIKIA HIVI PUNDE NI KWAMBA KATIBU MKUU WA TFF ANGETILEH OSIAH AMELAZWA KWENYE HOSPITAL YA AGA KHAN...TUTAKULETEA TAARIFA ZAIDI KUHUSIANA NA AFYA YAKE!

TUNAKUOMBEA UPONE HARAKA KAKA YETU NGETA ILI UWEZE KUREJEA NA KULIJENGA TAIFA LETU.

ETI HUYU NI NANI ?

Na Mwandishi Wetu

Abdalah Mohamed 'Prins Naseem KUTETEA UBINGWA WAKE NA Salehe Mkalekwa
.Februari 24
BINGWA wa mkanda wa Shirikisho la ngumi za kulipwa Tanzania (PST)
Abdalah Mohamed 'Prins Naseem' atapanda ulingoni kutetea mkanda wake
wa PST Februari 24 mwaka huu dhidi ya Salehe Mkalekwa.
Pambano hilo la ubingwa wa PST litakuwa ni pambano la uzito wa kg 57
na litashirikisha mapambano mengine manne ya utangulizi.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mratibu wa pambano hilo Shaban Adiosi
'Mwayamwaya' alisema pambano hilo litafanyika katika ukumbi wa New
Kibeta uliopo mbagala kuu Dar es Salaam.
Alisema pambano hilo la ubingwa wa PST ni muendelezo wa shirikisho
hilo kuendelea kuwainua mabondia chipkizi ambao hawajawa na majina
makubwa ili nao waweze kufikia kiwango kizuri cha mchezo huo.


"Ubingwa huu wa PST ni maalum kwa ajili ya mabondia chipkizi na ndio
maana mabondia wanaoshirikishwa wengi ni chipkizi na lengo ni
kuendeleza vipaji vyao,"alisema Mwayamwaya.
Aliyataja mapambano ya utangulizi yatakayopamba pambano hilo yatakuwa
kati ya Shaaban Zungu na Hasan Salehe watakaopigana uzito wa kg 55,
Safari Mbeyu na Ibrahim Maokola watakaopigana uzito wa kg 67, Jofrey
Pacho atakayetwangana na Seleman Shaaban na Abdalah Yusuph
atakayepigana na Omari Kijepa.
Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye
mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth,
Roy Jones na wengine kibao ‘DVD’ hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali
ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha Rajabu Mhamila
‘Super ‘D’.

“Ninatarajia kuwapelekea DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika
pambano kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo
wa ngumi,” alisema Super ‘D’



Kocha wa mchezo wa ngumi Saba Joseph (kulia) akimwelekeza bondia Saleh
Mkalekwa jinsi ya kutupa masumbwi katika kambi yake iliyopo Mbagala
Mkalekwa anajihandaa na mpambano wa ubingwa wa PST na Abdalah Mohamed
'Prins Naseem' Februari 24.(Picha na
www.superdboxingcoach.blogspot.com)

Friday, February 3, 2012

MANCINI ALA MATAPISHI YAKE-ASEMA TEVEZ ANAWEZA KUICHEZEA TENA CITY

Kocha wa Manchester City Roberto Mancini amekiri Carlos Tevez anaweza kucheza tena katika kikosi chake ikiwa atamshawishi kwamba yupo fit .
Japokuwa na imani kubwa iliyokuwa imetawala kwamba mshambuliaji huyo mwenye miak 27 angekuwa ameshaondoka City katika kipindi cha usajili, Tevez amebaki na City baada ya timu kama AC Milan, Inter Milan, na PSG kufaeli kumsaini kwa dili la kudumu.
Tevez kwa sasa bado yupo Argentina na kumekuwa hakuna uhakika wowote Carlitos atarejea lini England.

Japokuwa, Mancini ambaye siku za nyuma aliwahi kusema haifikiriki kwa Tevez kuvaa tena jezi ya Man City, lakini sasa muitaliano huyo amemtaja Carlitos katika majina ya wachezaji 25 watakaotumika katika premier league.

“Carlos sio chaguo kwa sasa lakini inawezekana huko mbeleni akarudi kucheza hapa,” alisema Mancini.

“Nina matumaini kwamba amekuwa akifanya mazoezi katika kipindi cha miezi 3 iliyopita.

“Kuna kitu kimoja tu katika kichwa changu , kombe la Barclays premier league. Lakini akirudi na kama yupo fit – theninawezekana akapata nafasi katika kikosi.

FERGUSON: NI MUDA WA KUWAFUNGA CHELSEA UWANJANI KWAO SASA


Alex Ferguson amekiri sasa ni muda sahihi kwa Manchester United kumaliza rekodi yao mbaya katika uwanja wa Stamford Bridge.

Fergie hajawahi kuifunga Chelsea ugenini katika Premier league tangu 2004 na amepata pointi 3 kutoka katika 27 @Stamford Bridge.
Boss huyu wa United alisema: “Tumefanya vizuri sana ugenini msimu huu na tunahitaji kuendelea kufanya vizuri hata sasa.

“Tuna michezo muhimu ya ugenini muhimu mno katika mbio hizi za ubingwa – Chelsea, Tottenham na City.
“Mechi dhidi ya Chelsea katika miaka ya karibuni zimekuwa ngumu sana na tuna bahati mbaya sana pale Stamford Bridge. Wachezaji wangu wanajua nini cha kufanya.”

United wapo sawa kwa pointi na City katika msimamo wa ligi kuu ya England.
Wamepunguza pengo la pointi japokuwa na wakati mgumu walionao kutokana na majeruhi kuwa wengi katika kiksi chao, na sasa inaonekana watarudi katika form yao ya mwanzoni mwa msimu kwa wachezaji wengi wanaanza kurejea.

Fergie ana matumaini mtoto wa maajabu Tom Cleverley, 22, yupo tayari kurudi dimbani tangu alipopata majeruhi katika mechi dhidi ya Bolton mwezi September mwaka jana.
Ferguson : “Alikuwa hatari mwanzoni mwa msimu na itakuwa kama tumesajili mchezaji mpya kwa kuwa na Tom katika kikosi chetu. Nafikiri ni Cleverley ni mchezaji muhimu na anatafanya mabadiliko makubwa katika mbio za ubingwa.”

RIO FERDINAND: SIUTAKI UNAHODHA WA ENGLAND


Rio Ferdinand amejitoa katika mbio za watu wanaotajwa kuweza kumbadili John Terry kama Naohdha wa England.
John Terry alivuliwa kitambaa cha unahodha leo asubuhi ikiwa ni mara ya pili katika maisha ya soka.
Rio Ferdinand ndiye aliyekuwa mrithi wa Terry mara ya kwanza alipovuliwa unahodha, lakini Manchester United defender amesema hataki hata kufukiriwa katika watu wanaopaswa kuchukua jukumu hilo la unahodha safari hii.
“Sitaki kuwa nahodha wa England baada ya yaliyotokea kipindi kilichopita,” Ferdinand alisema katika ukurasa wake wa Twitter.
“(I) Nataka kuweka umakini wangu katika kuichezea United na ikiwa nitachaguliwa katika kikosi cha England nitakuwa mwenye furaha.”
Na katika interview fupi iliyorushwa na BBC Rio alikaririwa akisema: “Nimeshakuwa nahodha wa England hapo nyuma kwa kipindi kifupi. Nilinyang’anywa kitambaa cha unahodha na kwa sasa nataka ni-concentrate katika kuitumikia United, kiukweli . Napenda sana kuichezea vizuri Manchester United.”
Ferdinand alikuwa aiongoze England katika kombe la dunia 2010 lakini akapata maumivu ya goti yaliyomuweka nje ya michuano hiyo

Ferdinand alikasirishwa na jinsi alivyotendewa na Capello wakati unahidha aliporudishiwa Terry mwaka mmoja uliopita huku mlinzi huyo wa United akiwa hajataarifiwa kuwa ameporwa unahodha huo.

HAPPY BIRTHDAY: ATHUMAN IDD MACHUPPA ' BOTTLE '

                   MACHUPPA AKIWA NA CREDO MWAIPOPO




                           HAPA YUPO NA DOGO...

Aliyekuwa Refa wa Kimataifa Gratian Matovu amefariki Dunia leo

Aliyekuwa Refa wa Kimataifa hapa nchini, Gratian Hemans Matovu (pichani), amefariki dunia leo jijini Dar es Salaam. Kwa mukujibu wa mtoto wake Bw. Stephen Matovu, Mzee Matovu amefariki leo majira ya saa 6 mchana huko nyumbani kwake Mbezi Beach (Makonde) na taratibu za mazishi zinaendelea hapo hapo nyumbani kwake. Mzee Gratian Matovu alianza kuwa refarii wa kimataifa tokea miaka ya 1964 na aliendelea na shughuli hiyo hadi miaka ya 1970 na hadi Mwaka 2006 alikuwa bado katika Kamati ya Marefarii Tanzania. HISTORIA FUPI Mzee Matovu alipata Diploma ya Urefarii kunako miaka ya 1956 na akaja kuwa refarii Daraja la Kwanza mnamo Mwaka 1961. Miaka Mitatu baadae alipata Beji ya FIFA. Mzee Matovu alipata kushika nyadhifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na Rais wa Chama cha Marefarii Tanzania.
Kwa Taaria zaidi za wasiliana na STEPHEN MATOVU 0713576666
Mungu Amlaze Mahala Pema Peponi Amina

SOFIA MWASIKILI : ' MUNGU AKIJALIA KESHO NACHEZA MCHEZO WANGU WA KWANZA KWENYE SOKA LA KULIPWA '


SOFIA MWASIKILI AKIWA NA WACHEZAJI WENZAKE NCHINI UTURUKI.

HIKI NDO KIKOSI CHA LULEBURGAZGUCU




kesho Mtanzania Sofia Mwasikili anatarajia kucheza mchezo wake wa kwanza tangia ajiunge na timu yake ya LULEBURGAZGUCU ya nchini Uturuki dhidi ya timu ya konak bel.
Luleburgazgucu inaongoza ligi  kuu ya wananwake ya nchini Uturuki ikiwa na Pointi 24 huku Konak bel ikishika nafasi ya pili na pointi 15. ligi hiyo inashirikisha jumla ya timu sita.

Official: Mtibwa Sugar Yamsimamisha Mecky Mexime.

Taarifa kutoka huko mkoani Morogoro zinasema kocha msaidizi wa Mtibwa Sugar FC. Meck Mexime amesimamishwa baada ya wachezaji kumkataa
taarifa inasema wachezaji wa Mtibwa Sugar walikua na mgomo baridi uliosababisha timu hiyo kupoteza michezo miwili mfululizo kwenye uwanja wake wa manungu dhidi ya JKT Oljoro na Coastal Union .
baada ya uongozi wa juu wa Kiwanda kukaa na wachezaji hatimae wachezaji hao wakasema hawamtaki ndani ya timu. Na ndipo utawala wa kiwanda ukaamua kumsimamisha kazi pamoja na wachezaji wengine wawili.

EXCLUSIVE: DAVID DE GEA KUSIMAMA LANGONI DHIDI YA CHELSEA


David De Gea yupo tayari kutoa suluhisho la tatizo la golikipa katika kikosi cha Manchester United at Stamford Bridge baada ya kuitumia siku ya alhamisi kumshawishi Sir Alex Ferguson kuwa yupo fit kwa kufanya session mbili za mazoezi.
Ferguson alikuwa na hofu kumuanzisha the 21-year third choice keeper Ben Amos katika mechi ya Jumapili dhidi ya Chelsea, baada ya De Gea kuumwa ghafla huku Anders Lindegaard akiumia enka.
Lakini jana De Gea alirudi mazoezini na kumpa ahueni Fergie, hivyo mhispania huyo atasimama langoni siku ya Jumapili.

MTIHANI WA MAWAKALA WA WACHEZAJI

MTIHANI WA MAWAKALA WA WACHEZAJI


Mtihani wa uwakala wa wachezaji (players agent) wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utafanyika Alhamisi ya Machi 29 mwaka huu saa 10 kamili asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

 Kutakuwa na jumla ya maswali 20 kwenye mtihani huo, 15 yanatoka FIFA kuhusiana na kanuni za kimataifa za mpira wa miguu na matano yatatoka TFF kuhusiana na kanuni mbalimbali zinazotawala mchezo huo nchini.

Kwa ambao wangependa kufanya mtihani huo utakaokuwa katika lugha ya Kiingereza wanatakiwa kujisajili TFF kwa ada ya dola 50 za Marekani ambapo watapewa utaratibu na maeneo ambapo mtihani huo unalenga.

Muda wa kufanya mtihani hautazidi dakika 90. Mtihani uliopita ulifanyika Septemba 29 mwaka jana ambapo watahiniwa wanane walijitokeza na kufanya mtihano huo.

 Mpaka sasa Tanzania ina mawakala saba wa wachezaji wanaotambuliwa na FIFA. Mawakala hao ni Ally Mleh wa Manyara Sports Management, Damas Ndumbaro, John Ndumbaro, Mehdi Remtulla, Ally Saleh, Yusuf Bakhresa na Said Tully.


RAUNDI YA 16 LIGI KUU YA VODACOM


Mzunguko wa 16 wa Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara unaanza kesho (Februari 4 mwaka huu) kwa mechi tatu. Coastal Union itakuwa mgeni wa Moro United kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam.

Nayo Villa Squad itakuwa mwenyeji wa Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Ruvu Shooting na Polisi Dodoma zitaoneshana kazi kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani.

Viingilio kwa mechi ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam vitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya bluu na kijani, sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP B na C, sh. 15,000 kwa VIP A wakati Uwanja wa Chamazi ni sh. 10,000 kwa Jukwaa Kuu na sh. 3,000 mzunguko.

Kwa mechi ya Mlandizi kiingilio ni sh. 2,000 kwa mzunguko wakati Jukwaa Kuu itakuwa sh. 5,000. Pia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefanya mabadiliko ya muda wa kuanza mechi za ligi hiyo kwa kituo cha Dar es Salaam. Mechi zinazochezwa wikiendi kwenye Uwanja wa Taifa zitaaza saa 10 kamili jioni wakati zile zinazochezwa siku za kazi zitaanza saa 10.30 jioni. Mechi zote za Uwanja wa Azam- Chamazi zitaanza saa 10 kamili jioni.


MZUNGUKO WA PILI LIGI DARAJA LA KWANZA (FDL)


Mzunguko wa pili (second leg) wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inayochezwa katika makundi matatu tofauti unaanza kesho (Februari 4 mwaka huu) kwa mechi sita. Katika kundi A, Morani FC itakuwa mwenyeji wa Burkina Faso ya Morogoro katika mchezo utakaochezwa Kiteto mkoani Manyara.

Kwa upande wa kundi B timu zote sita zitakuwa uwanjani. Small Kids ya Rukwa itacheza na Polisi ya Iringa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, Mbeya City na Tanzania Prisons zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya na Majimaji na Mlale JKT watapepetana katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Kundi C litaanza kwa mechi mbili ambapo AFC ya Arusha watakuwa wageni wa Manyoni mkoani Singida na Rhino na Polisi Tabora zitakwaruzana kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora. Mechi nyingine ya kundi hilo itakuwa kati ya 94 KJ na Polisi Morogoro ambayo itachezwa keshokutwa (Februari 5 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani.


SIMBA, OLJORO JKT ZAINGIZA MIL 40


Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Oljoro JKT lililochezwa Februari Mosi mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 40,191,000. Jumla ya watazamaji waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 105 kwa kiingilio cha sh. 3,000, sh. 5,000, sh. 10,000 na sh. 15,000 kwa VIP A walikuwa 11,860.

Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kila timu ilipata sh. 7,023,171, uwanja sh. 2,341,057, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 936,423, TFF sh. 2,341,057, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,170,528 na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh. 234,106.

Nayo mechi namba 104 kati ya African Lyon na Polisi Dodoma iliyochezwa Februari Mosi mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam imeingiza sh. 45,000 kutokana na watazamaji 15 waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo. Baada ya kuondoa asilimia 18 ya VAT ambayo ni sh. 6,864.41 kila timu ilipata sh. 2,591, Uwanja sh. 514, TFF sh. 514, DRFA sh. 205, FDF sh. 257 na BMT sh. 51.

BREAKING NEWS: JOHN TERRY AVULIWA UNAHODHA WA ENGLAND


John Terry amevuliwa unahodha wa timu ya Taifa ya England kwa mara pili katika maisha yake ya soka.
Terry aliitwa na leo saa 4 asubuhi na Mwenyekiti wa FA David Bernstein na kuambiwa uamuzi uliochukuliwa na bodi ya maamuzi ya FA.
Uamuzi huu FA utakuwa umemuudhi kocha Fabio Capello ambaye yeye siku zote amekuwa akimtetea Terry na aliweka wazi ndiye atakayekuwa nahodha wa England katika EURO 2012.
Pia FA imempa muda wa kufikiria Terry kama bado anataka kuiwakilisha timu yake ya taifa katika EURO, lakini wamesema hatolazimishwa kufanya maamuzi kwa haraka.

Debate:Sekretariet ya TFF ilikuwa wapi toka kipindi hicho kuomba mwongozo hadi wasubiri leo uchaguzi wa DRFA umetangazwa ?

Kamati ya rufaa ilishatoa hayo maamuzi muda mrefu siku chache baada ya uchaguzi wa Mara kufanyika , sasa Sekretariet ilikuwa wapi toka kipindi hicho kuomba mwongozo hadi wasubiri leo uchaguzi wa DRFA umetangazwa na Wambura alionyesha nia ndio wanaomba mwongozo?

Kwasasa Cristiano anataniwa kuwa CR7 =Cristiano Penaldo 7 au Penotric


Je wajua ukweli? Cristiano Ronaldo ndiye mchezaji aliyeweka rekodi kwenye LA LIGA kwa kufunga magoli mengi ktk nusu ya kwanza ya msimu, ambapo mabao 7 kati ya hayo mabao 24 ameyafunga kwa njia ya PENALTI. Ameweka rekodi ya kufunga magoli ya penalti nyingi zaidi miongoni mwa wafungaji bora waliowahi kuweka record ya ufungaji bora kwenye LigaBBVA. Mpaka sasa  ktk magoli 24 aliyofunga magoli 7 ni kwa njia ya penalti. Mpaka mwishoni mwa msimu uliopita  alikuwa amepewa zaidi ya magoli 10 ya penalti. Vilevile kati ya magoli 22 alofunga Messi goli 1 tu ndo lilikua la penalti. Kwasasa Cristiano anataniwa kuwa CR7 =Cristiano Penaldo 7 au Penotric. Source [él comfidèntial 2011].


KUTOKA KWA MDAU BRYSON SABUNI!

TAKWIMU MBALIMBALI ZA LIGI KUU YA ENGLAND MPAKA SASA.




Thursday, February 2, 2012

RATIBA YA ROBO FAINALI YA AFRICAN CUP OF NATIONS 2012


Quarter-finals

4 February 2012
17:00
Zambia v Sudan

4 February 2012
20:00
Côte d'Ivoire v Equatorial Guinea

5 February 2012
17:00
Gabon v Mali


5 February 2012
20:00
Ghana v Tunisia

BREAKING NEWS: FA WAKUTANA LEO KUZUNGUMZA JUU YA UNAHODHA WA JOHN TERRY KATIKA KIKOSI CHA ENGLAND.


Saa chache baada ya moja ya wachezaji wa zamani Jason Roberts kusema John Terry ni sumu katika kikosi cha England, viongozi wa chama cha soka cha England FA wanaweza wakaamua kumvua  kitambaa cha unahodha Terry leo hii Ijumaa.
Mwenyekiti wa FA, David Bernstein amewasiliana na wanachama  12 wa bodi ya juu ya maamuzi jana Alhamisi kusikiliza mawazo yao juu ya suala la Terry.
Inavyoonekana wengi wa wanachama wa bodi hiyo hawadhani kama ni jambo sahihi kwa Terry kuwaongoza waingereza katika EURO 2012 huku akiwa na mashtaka ya matusi ya kibaguzi wa rangi, na wanaona FA kwa haraka inabidi ifanya maamuzi haraka kabla ya mkutano wa February 23 mwaka huu.

GIGGS: TUKIVUKA MWEZI HUU SALAMA TUNACHUKUA TENA UBINGWA.


Ryan Giggs anaamini kombe litabaki Old Trafford ikiwa Manchester United wataupita vizuri huu mwezi.
United watawatembelea Chelsea Jumapili hii, baadae watakutana na Liverpool na Tottenham, huku wakifunga mwezi huu kwa mechi ya ugenini dhidi ya Norwich.
Vijana wa Sir Alex Ferguson waliwakamata City kileleni wiki hii baada ya kuwafunga Stoke.
Na veteran huyu mwenye makombe 12 ya premier leaguae, Giggs anajua thamani ya kombe watakaloshinda kwa kuwashinda mahasimu wao wakubwa.
Alisema, “Tumeshaanza kurudi kwenye form yetu na kama tutapata matokeo mazuri katika michezo hii, confidence itakuwa juu sana.
“Tunafahamu ni mbio ngumu, lakini hiyo ndio michezo ambayo kila mtu anataka kucheza. Tunajua hii ni michezo muhimu sana, na tunafahamu kama tutashinda mechi hizi, then tutakuwa katika nafasi nzuri ya kuweza kuutetea ubingwa wetu.
“Tunajua kilicho mbele yetu na nini tunapaswa kufanya.”

ENDAPO JOHN TERRY ATAENDA EURO 2012: KIKOSI CHA ENGLAND KITAGAWANYIKA

Chama cha soka cha England kimeonywa juu ya sumu inayowezwa kusambazwa katika timu ya taifa ya England ikiwa John Terry ataitwa na kwenda katika michuano ya EURO  2012.
Terry anatuhumiwa kumtukana kwa kumtolea maneno ya kibaguzi Muingereza mwenzie Anton Ferdinand na kesi yake amabyo ilitajwa jana imepangwa kusikilizwa July 9, tarehe ambayo itakuwa baada ya kumalizika kwa michuano ya EURO.
Lakini Jason Roberts, mchezaji wa zamani wa Blackburn ambaye amehamia Reading na pia ni maarufu kama mchambuzi wa soka katika radio, anasema Terry hapaswi kuitwa na inabidi aondolewe katika kikosi cha England atleast mpaka kesi yake ya ubaguzi itakapoisha.
Pia anasisitiza hoja ya boss Fabio Capello kuwa Terry hapaswi kuhukumiwa kabla hajapatikana na hatia sio sahihi kwa kesi hii kwa sababu hata kaka yake Anton alitimuliwa katika kikosi cha ENGLAND kabla hajapatikana na hatia na FA kwa kukacha kupima vipimo vya matumizi ya madawa.
Akiwa katika mtandao wa Twitter, Roberts aliseama: “Nimeona kesi ya Ferdinand  na Terry imesogezwa mbele. Siamini kama ni sahihi kwa nahodha wa England kwenda katika Euros.
 “Msemo wa hakuna hukumu kabla ya kupatikana na hatia haufanyi kazi mara zote katika soka kama ilivyokuwa kwa Rio Ferdinand in 2003. Pia muhimu zaidi, naamini dressing room ya England at EUROS itakuwa imegawanyika na hiyo inaweza ikawa sumu.”
Situation ya Terry inaweza kuzungumziwa katika kikao kijacho FA.
Lakini inaeleweka Capello anataka kumchukua Terry kwenda nae EURO kama kiongozi wa timu.
Macho yote sasa yategeukia @Stamford Bridge jumapili hii ambapo Terry anakutana na Rio Ferdinand wa Manchester United kaka wa Anton.
The Premier League committee imesema utaratibu wa kupeana mikono utaendelea kama kawaida katika mechi hiyo – tofauti na walivyofanya FA katika mchezo wa Carling cup kati ya QPR na Chelsea.

FIFA: TUNAHITAJI RIPOTI NZIMA YA TUKIO LA VURUGU MISRI


Shirikisho la soka duniani FIFA limeomba kupatiwa ripoti nzima ya tukio la vurugu lilitokea nchini Misri ambalo limeacha watu zaidi ya 70 kufariki dunia.
FIFA imetoa amri kwa mamalaka ya soka  nchini Misri kuelezea kila kitu nini kilitokea katika mechi kati ya AL-Ahly na AL Masry jana jumatano.
Raisi wa FIFA Sep Blatter amemwandikia raisi wa FA ya Misri Samir Zaher.
“Leo ni siku nyeusi katika soka na lazima tuchukue hatua kuhakikisha tukio kama lile halijirudii tena. Soka ni mchezo wa nguvu zinazotumika kwa mazuri na lazima tusiruhusu zitumike vibaya kwa wale wenye mambo mabaya. Nasubiri habari zaidi kuhusu tukio lile.”
Maofisa wakubwa katika chama cha soka cha mji wa Port, ambapo ndipo tukio hilo lilipotokea , na viongozi wengine wa FA tayari wameshafukuzwa kazi.
Pia gavana wa mji wa Port ameshajiuzulu huku maofisa wawili wa juu wa usalama tayari wakiwa washasimamishwa na wapo chini ya ulinzi.
Siku 3 za maombelezo zimetangazwa na serikali. Pia kutakuwa na muda wa kukaa kimya katika mechi za robo fainali za African cup of Nations.