Search This Blog

Loading...

Saturday, March 17, 2012

SWALI LA KIZUSHI KATI YA CHUJI NA KISAMBELE NANI MKUBWA ?

NINAVYOFAHAMU PIUS KISAMBALE NA ATHUMAN IDD  'CHUJI' NI NDUGU WA TUMBO MOJA, HUKU ATHUMANI IDD AKIWA AMEZALIWA TAKRIBANI MIAKA MIWILI KABLA YA PIUS. SWALI LA KUJIULIZA IMEKUAKUAJE HIVI SASA PIUS AMEKUA KAKA WA ATHUMAN ? JE? NI WAPI ATHUMAN ALIKWAMA UMRI MPAKA PIUS AKAJA KUMPIKU ?
NAMEPIUS KISAMBALE
NATIONALITYTANZANIA
DATE OF BIRTH21 DECEMBER 1987
HEIGHT5’8’ INCHES
WEIGHT68KGs
POSITIONSTRIKER
JERSEY11
PREVIOUS CLUBPolisi Dodoma, Prison FC,
Simba SC    
Polisi FC (Rwanda),              
Goha FC (India),
Moro Utd, Mtibwa Sugar, Ruvu JKT

NAMEATHUMAN IDD
NATIONALITYTANZANIA
DATE OF BIRTH 18 FEBRUARY 1988
HEIGHT
WEIGHT
POSITIONMIDFILEDER
JERSEY18
PREVIOUS CLUBPolisi Dodoma, Simba SC

TAARIFA KUTOKA TFF!

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Machi 18, 2012

SEMINA ELEKEZI COPA COCA-COLA MACHI 25
Semina elekezi kwa ajili ya mashindano ya Copa Coca-Cola 2012 itafanyika Machi 25 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo washiriki ni makatibu wakuu wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa au wawakilishi wao ambao wanatakiwa kuwa na utambulisho rasmi.

Washiriki kutoka nje ya Mkoa wa Dar es Salaam wanatakiwa kuwasili Machi 24 mwaka huu na watapokelewa katika hoteli ya Itumbi iliyoko Magomeni-Mwembechai.

TFF itawagharamia washiriki kwa chakula, malazi na nauli za kuja Dar es Salaam na kurudi kwa usafiri wa basi au meli.

Michuano ya mwaka huu itaanza Machi 31 hadi Mei 5 katika ngazi ya wilaya. Usajili kwa ngazi ya mkoa utaanza Mei 6 hadi 15 wakati mashindano yake yatafanyika kuanzia Mei 16 hadi 25.

Usajili na maandalizi kwa michuano ya ngazi ya Taifa utaanza Mei 26 hadi Juni 7. Usajili wa timu za mikoa unatakiwa kuwasilishwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kati ya Juni 8 na 14 mwaka huu.

WANYARWANDA KUCHEZESHA SIMBA, ES SETIF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limewateua waamuzi kutoka Rwanda kuchezesha mechi ya kwanza ya raundi ya kwanza kuwania Kombe la Shirikisho kati ya Simba na ES Setif itakayochezwa Machi 25 mwaka huu.

Mwamuzi wa kati ni Hudu Munyemana wakati wasaidizi wake ni Felicien Kabanda, Theogene Ndagijimana na Edouard Bahizi. Kamishna wa mechi hiyo ni Felix Tangawarima kutoka Zimbabwe.

Mechi hiyo namba 45 itafanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni. Mechi ya marudiano ambayo ni namba 46 itachezwa Aprili 6 mwaka huu nchini Algeria.

Iwapo Simba itafanikiwa kusonga mbele itacheza mechi ya kwanza nyumbani Aprili 29 mwaka huu na mshindi kati ya El Ahly Shandy ya Sudan na Ferroviario de Maputo ya Msumbiji ambapo ya marudiano itachezwa kati ya Mei 11, 12 na 13 mwaka huu.


Powered by Sorecson : Creation de site internet
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

HATUA TANO KABLA YA BAO LA YANGA DHIDI YA VILLA SQUAD.

Hii ndiyo hatua ya tano la goli la Yanga dhidi ya Villa

 Kipa wa Villa Sguad Daud Mwasongwe akiwa amelala chini akishuhudia namna ambavyo mshambuliaji wa Yanga Pius Kisambare anaondoka na mpira kabla ya kutoa pasi kwa Hamisi Kiiza na kufunga bao la ushindi huku beki wa Villa Gerald Lukindo akishangaa mashabiki jukwaani wakati wa mechi ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Yanga ilishinda bao 1-0


Hii ndiyo hatua ya nne kabla ya Kiiza kufunga goli dhidi ya Villa

Mshambuliaji wa Yanga Pius Kisambare akichukuwa mpira mgongoni mwa Kipa wa Villa Sguad Daud Mwasongwe baada ya Kipa huyo kuanguka chini kabla ya kumpa Hamisi Kiiza pasi na kufunga bao la ushindi.

Hii ndiyo hatua ya tatu la goli la Yanga dhidi ya Villa

Mpira ukiwa mgongoni mwa Kipa wa Villa Squad huku mshambuliaji wa Yanga Pius Kisambare akijaribu kuuwania kabla ya kumpa  Hamisi Kiiza pasi na kufunga bao.
Hatua ya pili la goli la Yanga dhidi ya Villa

 Mpira ukimponyoka Kipa wa Villa Squad Daud Mwasongwe kichwa ni mwa mshambuliaji wa Yanga Pius Kisambale uku Hamisi Kiiza wa yanga akijiandaa kumsaidia.

Hii ndiyo hatua ya kwanza ya goli la Yanga dhidi ya Villa

Kipa wa Villa Sguad Daud Mwasongwe akidaka mpira kichwani mwa mshambuliaji wa Yanga Pius Kisambare huku Hamisi Kiiza akijiandaa kumsaidia wakati wa mechi ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

 kwa hisani ya http://www.japotz.com/

FABRICE MUAMBA AZIDIWA -HALI YAKE NI MBAYA SANA. BOLTON WATHIBITISHA.

Kiungo wa Bolton Fabrice Muamba yupo katika hali mbaya zaidi akipigania maisha yake katika chumba cha ICU, katika kituo cha magonjwa ya moyo ndani ya Hospitali ya Chest, London, klabu yake imethibitisha.
Madaktari wakiwa wanahangaika kuokoa maisha ya

Kiungo huyo mwenye miaka 23 alianguka ghafla katika mechi ya raundi ya sita ya kombe la FA dhidi ya Tottenham  na akapewa huduma ya kuushtua moyo pale pale uwanjani.
Gareth Bale akiwa anamfariji mchezaji mwenzioe Defoe.

Mapema jioni ya leo hii baada ya kuanguka, iliripotiwa kwamba hali yake imeimarika, lakini sasa Bolton wametoa tangazo rasmi.
Huku mechi ikiwa 1-1, mchezaji huyo wa kikiso cha England under 21 alionekana akidondoka na mara moja madaktari wa timu zote mbili waliamua kushirikiana kujaribu kuokoa maisha yake.
Van Der Vaart akiomba dua kwaajili ya Muamba.

Baada ya kutibiwa kwa dakika 6 dimbani Muamba alichukuliwa na machela akiwa amefungwa oxygen na kupelekwa hospitali kwa matibabu zaidi.
Kutokana na tukio mechi hiyo iliaghirishwa.
Zilisomwa dua nyingi katika kuhikisha Muamba anarudia afya yake.

HUYU NI NANI: KIPA MFUPI KULIKO WOTE DUNIANI?TIP